mmmmh


oo

Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

nifanyaje uridhike

Chonde chonde niambie, nini unachokitaka,
Kingine nikufanyie, ambacho utaridhika,
Niambie nitulie, nimechoka kuteseka,
Nifanyeje uridhike, nambie basi nijue.

Ulitaka yako nyumba, nyumba nayo nikajenga,
Mkopo nikaubamba, wewe uache kupanga,
Ukakataa Kibamba, hutaki wala Ukonga,
Ukataka Mikocheni, nikakopa uridhike.

Nikasema njoo Mbeya, haraka ukakataa,
Ukadai ni kubaya, wataka kuishi Dar,
Nami nikasema haya, nikuridhishe haswaa,
Bado wataka Ulaya, Dar hapajakufaa.

Mara ukataka gari, huzitaki daladala,
Tena gari la fahari, hutaki hizo Corolla,
Nikuridhishe vizuri, nikaenda kopa hela,
Gari umeshalipata, wasema hujaridhika.

Nguo nzuri uzipate, likawa lako sharti,
Tena Mlimani City, vinginevyo varangati,
Kabidi nijikung’ute, ‘sije kukuudhi switi,
Nami pesa nikakopa, nguo uweze nunua.

Ukataka simu kali, bei yake milioni,
Tena ukataka mbili, zote ziwe iPhone,
Waijua yangu hali, lakini hatwelewani,
Simu hizo nimekupa, bado wataka vingine.

Ukataka iPad, laptop huitaki,
Nami nikajitahidi, nikakopa pesa benki,
Nikuridhishe waridi, moyoni ‘lotamalaki,
Wasema huna furaha, bado sana kuridhika.

Ndege ukataka panda, tena ya Lufthansa,
Eti unachokipenda, kutalii Ufaransa,
Moyo sasa wanidunda, utadhani nina kansa,
Sikai nikatulia, mahabuba huridhiki.

Nimefanya kila jambo, nadhani nakuridhisha,
Kumbe wafata mkumbo, wapo wanokufundisha,
Nateseka joto tumbo, mwenzangu unajirusha,
Nini zaidi nifanye, nawe uache nitesa?

visitors comments