mmmmh


oo

Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

BARUA ZA MAPENZI

Mwaaa
Habari zako , za moyo wako , za tabasamu lako , za kicheko chako , sauti yako na kila kitu kizuri chako ? Najua kila kitu kitakuwa safi sana kuanzia moyo wako mzuri na mtamu uliojaa upendo na mapenzi ya dhati kabisa ulio mkweli na mvumilivu . Angalia ndani ya moyo wako , utakuta hakuna kitu cha kuficha , pengine unaweza kuficha kwa sababu ni wajibu wa kila mtu katika maisha yake , lakini linapokuja suala la kupendana basi mambo ya kuficha hakuna tena kama ukiwa na uhakika kuhusu uhusiano wako . Nikifikiria kuhusu wewe , nafikiria kuhusu dunia ya mapenzi iliyo nyooka na iliyo katika njia sahihi kabisa , mpaka hapo jua tu mimi na wewe mpaka milele kwenye mabonde twendeDear ,

, baharini tuogelee hata hewani tutapaa . Tabasamu lako ambalo ndio nalipenda zaidi , na kila mara huwa nalihisi liko mbeleni mwangu lakini kama unavyojua muda mwingi uko mbali najaribu kufikiri tu je kama tungekuwa tuko wote masaa 24 siku 7 usiku na mchana sijui ningesema maneno gani kusema za ukweli namisi tabasamu lako maridani Kicheko chako ambacho nikisikia moyo wangu huenda kasi kuliko wakati wowote ule , Dear labda nikuambie kitu Fulani , mimi napenda sana kusikia vicheko , unajua kuna wakati ukiwa sehemu Fulani Fulani jinsi unavyocheka ndio watu wale wanavyoweza kukuweka katika kundi gani , wewe kicheko chako nakuweka katika kundi la wanadamu maridani . Hiyo sauti yako ni zaidi ya Coco Lee , honey kama hujui au hujawahi kusikia , Coco Lee ndio mwanamuziki wa kike mwenye sauti ya mvuto zaidi duniani mpaka sasa hivi , moja ya nyimbo nzuri kabisa aliimba na Julio Iglesius inaitwa WHEN U TELL ME THAT U LOVE ME kwahiyo wewe ni zaidi yake , pengine ungeamua kuimba leo ningekuwa naandika kuhusu kitu kingine cha zaidi . Honey huwa napata furaha sana kila ninapopata wasaa wa kukuandikia email , kila ninapopata nafasi ya kukusalimia wewe , wengine hawapati nafasi hii kutokana na sababu zao mbali mbali , wengine hawana mikono ya kuandika , wengine wameachana na wapenzi wao , wengine wamegombana na wapenzi wao na kadhalika lakini mimi nafurahi nakuandikia email hii kwa furaha kuu kuliko zote . Kikomo naishia hapa , naomba tuendelee kuwasiliana siku nyingine tena , mwisho wa barua moja ndio mwanzo wa barua nyingine nzuri na bora zaidi , kwahiyo usijali sana mrembo wangu .
Natamani ningekuwa kengele
Ningelia unisikie hapo ulipo

ni wako barafu wa moyo

♥••.¸¸.• mahabat •.¸¸.••♥

dear mpendwa
salaam sana ama baada ya salaam mi ni mzima hofu na mashaka kwako wangu kipenzi.

dhumuni ya barua hii ni kukujulisha nakupenda sana kwani we
we ni mwanaume wa pekee uliye uteka moyo wangu,usiku silali mwezio
mzimu wa penzi lako haliniachi nikalala,huwa nashukuru ninapopitiwa
na usingizi lakini bado ndoto hunisumbua .

kipoza cha moyo wangu ni wewe ,nakupenda sana.mwaaaaaaaaaaaaaa

wako sakafu wa moyo wako
♥••.¸¸.• mahabat •.¸¸.••♥
dear mpenzi

natumai yu mzima wa afya pamoja na mengineyo,ni yangu faraja kukuandikia barua hii ili
ujue ni kwa kiasi gani nakupenda wangu daktari.

Nakumbuka kwa ulimi wako mtamu ulinifundisha kuwa “akwambiae ndie akupendae.” Nlitaka kukwambia zamani dukuduku langu, tangu enzi zileee ulipokuwa ukilindwa na makomando lakini nikaogopa. Nisiogope? Naam niliogopa. Ningekwambia siku zile ungenikosa. Ungenitafuta usinijue nilipo. Hata ungeniona aahh wapi! Sifai. Ninyan’ganyan’ga. Hawakiambilika wale. Ila sasa nahisi ndio wakati muwafaka wa kukwambia. Na nakwambia ili ujirekebishe. Na nakwambia kwa kuwa nakupenda, wewe ni wangu wa milele. Nakwambia kwa kuwa naamini walinzi wako wapya waweza niruhusu nikwambie bila ya kunidhuru. Wao pia naamini wanaamini nnayokwambia ni muhimi kwako na kwa maslahi yao wao, watumishi wako.
♥••.¸¸.• mahabat •.¸¸.••♥
Mpenzi wangu,
Nikupendaye kwa dhati kutoka moyoni mwangu,
Nakusalia salamu ya huba iliyoambatana na busu motomoto.
Mpenzi wangu nianze kwa kukushukuru sana kwa barua yako iliyojaa huba ambayo nimeipokea jana mchana nikiwa kazini. Niseme tu nimefurahi sana mpenzi wangu kupata barua yako. Siku zote barua zako huwa tiba mahabuba moyoni mwangu. Kila niusomapo mwandiko wako wa kimahaba huwa napata liwazo la haja moyoni mwangu. Maneno ya kwenye barua yako ni dawa isiyo na kifani ndani ya moyo wangu. Kila mara najikuta moyo wangu unaongeza maradufu upendo juu yako.

Mpenzi wangu, usishangae kuwa nimepata barua jana lakini nimechelewa kukujibu hadi leo ndiyo nimeshika kalamu na karatasi ili nikuandikie ewe kipenzi cha moyo wangu. Nilipoipata barua yako nilitafakari kwa muda mrefu mno hadi kujikuta nikitokwa na machozi. Hayakuwa machozi ya furaha kama yale yanidondokayo kila wakati nisomapo maneno matamu kutoka kwako ewe mwandani wangu. Maneno ya kwenye barua yako yamenichoma moyoni mwangu mithili ya mkuki wenye ncha kali tena iliyoiva vilivyo kwenye tanuru la moto. Mpenzi wangu, niliyekuchagua mimi mwenyewe kutokana na hisia kali na mapenzi mazito sana niliyonayo moyoni mwangu juu yako, amini bado nakupenda sana.

Mpenzi wangu, nikakiri kwa yakini kuwa nilikuahidi toka miaka mingi sana kuwa pindi nitakapojaaliwa kupata kazi nitakuoa. Nayakumbuka maneno ya ahadi niliyokuwa nikikupa kila mara tulipokuwa tukipata kaupenyo ka kuwa pamoja. Ahadi yangu bado ipo pale pale mpenzi wangu. Moyo wangu, kwa dhati kabisa, bado una dhamira ya dhati ya kukuoa mpenzi wangu Kwenye barua yako umeandika jinsi unavyokata tamaa kwani sasa ni mwaka moja toka nianze kazi lakini sijatimiza ahadi yangu ya kukuoa. Mpenzi unaona kama nakupotezea muda na unaniomba kama sina haja nawe nikupe nafasi uolewe na mtu mwingine ambaye hata leo hii yupo tayari kuleta posa kwa wazazi wako. Sijui niyaelezeaje maumivu makali ninayoyasikia ndani ya moyo wangu.
Mpenzi wangu, niseme tu ukweli. Ninakupenda mno kuliko hata maana ya neno lenyewe upendo. Ninatamani sana hata sekunde hii hii niwe nimeoana nawe. Lakini, kama nikwambiavyo siku zote, ugumu wa maisha hapa Dar es Salaam hususani kwangu mie mfanyakazi wa kima cha chini ndiyo unaonifanya nikose uthubutu wa kukuoa ewe mpenzi wangu niliyekupa moyo wangu wote, haraka iwezekanavyo kama ambavyo nimekuwa nikikuahidi mara nyingi sana. Mpenzi wangu, moyoni mwangu inaniuma sana maana maisha magumu ninayoyaishi hapa Dar es Salaam kwa kweli yanatishia kwa kiasi kikubwa sana ustawi na uhai wa penzi letu.
Mpenzi wangu, nikwambie nini ili ufahamu kwa kiasi gani akili na moyo wangu vyatamani kwa dhati kabisa kuishi nawe milele yote kadri Mwenyezi Mungu atakavyotujaalia siku za kuishi humu duniani. Nikwambieje ili ufahamu ni namna gani nalitamani pendo hili lidumu humu duniani na baada ya hapo?
Mpenzi, maisha yangu mfanyakazi wa kima cha chini ni magumu mno. Fikiria mpenzi wangu, kamshahara kangu ambako ni kadogo mno, kanapaswa kalipe kodi ya nyumba, umeme, maji, matibabu, gharama za usafiri na mengineyo chungumbovu. Mpenzi wangu huwezi amini kuna wakati huwa nalazimika kutembea kwa miguu kutoka kazini pale Stesheni mjini hadi nilikopanga Mbagala Kizuiani. Huwa inanigharimu masaa karibia mawili nachapa tu mwendo tena wakati mwingine mvua ikininyeeshea mwili mzima. Sijakwambia tu mpenzi wangu, mara zingine huwa nalazimika kushindia mlo mmoja ama pengine nisile kabisa. We acha tu mpenzi wangu.
Mpenzi, natamani ningekuwa na uwezo wa kukufungulia moyo wangu uyaone yaliyo ndani. Natamani mno tena kupita maelezo kuoana nawe. Kinachonikwamisha mpenzi wangu ni ugumu tu wa maisha ninaokabiliana nao hapa mjini. Sikusudii kukuoa ili uteseke. Sikusudii kukuoa ili nikushindishe njaa. Siyakusudii hayo.
Mpenzi wangu, sikusudii kuuweka uhusiano wetu rehani. Mpenzi sina namna niwezayo kuibadili hali halisi kwa sasa zaidi ya kulazimika kufanya kazi kwa bidii ili pengine bosi wangu anione anipandishe cheo ama kunipa nafasi ya kwenda kujiendeleza kielimu. Lakini tatizo kazini kwetu kumejaa majungu mno kiasi kwamba uchapakazi wangu unanifanya nionekane kimbelembele. Kila mtu ananiona nina kiherehere hadi nalazimika kuwa mpole na goigoi kama wafanyakazi wengine. Kwa mtindo huu sijui ni lini nitafanikiwa kimaisha.

sitamani wala siombi uniache na kuolewa na mwingine kwa sababu tu ya hali yangu duni. Machozi yananitoka mno kuyaandika maneno haya. Ninakuomba mpenzi wangu univumilie walau kwa mwaka moja mwingine pengine serikali itatufikiria na kuamua kuboresha hali zetu. Chonde chonde mpenzi wangu.
Mpenzi wangu, najaribu kukwepa kuufikiria mtihani mkubwa unaokukabili kwa sasa. Mapenzi ya kweli ama maisha bora. Najaribu tu kupambana na wivu moyoni mwangu. Najaribu kutamani kuvivaa viatu vyako na kuchagua mapenzi ya kweli. Lakini sipungukiwi imani.
Mpenzi wangu, najua nimekuchosha kwa barua ndefu sana ambayo hata hivyo imeshindwa kujibu swali lako la nitakuoa lini. Ninatumai maelezo yangu pamoja na kutojibu moja kwa moja swali lako, angalau yametoa mwelekeo wa jibu.
Mpenzi wangu, natamani kusema mengi sana zaidi ya haya. Najua hata siku moja dau tupu haliendi joshi na maneno matupu hayajengi nyumba. Ninaloweza kukwambia ni kuwa ninakupenda mno, daima ninakuwaza wewe kwa kuwa umetamalaki moyoni mwangu. Wewe ndilo pambo la moyo wangu. Kwa huba na mahaba yajazayo vibaba na vibaba, penzi langu kwako limeshiba.
Nikupendaye daima,
Mpenzi wako.
♥••.¸¸.• mahabat •.¸¸.••♥

Salam,

Ama baada ya salamu, mimi ni mzima wa afya njema. Mie ni ndege nipo angani na nimetafuta mti wa kutua kila pembe ya dunia lakini sijaupata bado. Je naweza nikatua kwako?

♥••.¸¸.• mahabat •.¸¸.••♥

Asiyejua Kununa
P.o Box Mapenzi yalipozaliwa

Kwako wangu wa ubani AshaDii
Upatapo waraka huu elewa mie mwenzio sili silali
Upendo wangu kwako ni sawa na mchanga wa bahari.
Tupendane wanye wivu wameze wembe

Wako akupendaye mchana na usiku ABSQUARE

..................

Mpenzi wa Asiyejua kununa
S. L. P Mapenzi yalipotuliya

Kwako Kipenzi cha moyo na roho yangu,
mara baada ya kupata waraka huu akili imeruka kwa furaha,
hata niya ya kumkubali Slave aliyening'ang'ania kunitongoza
kama ruba kumeyeyeka kama barafu kwenye moto wa Petroli!

Mie nakupenda unipendae wenye wivu wacha wajinyonge
kwenye kamba ya radio cassete!

Wako akutunziae penzi la ukweli lisiloyumbishwa.

ADI.

Lol

♥••.¸¸.• mahabat •.¸¸.••♥
Usitie shaka kabisa kipenzi Smile.

Mie mzima kabisa wa afya, hofu na mashaka ni juu yako ulie mbali na uwepo wa macho yangu kama ilivyo kwa utosi na unyayo na kunifanya kujisikia kuumwa kila nikumbushwapo jina lako lililotawala kupitia smile ya wapendwa wangu wote. Natamani waendelee tu kununa. Lol

♥••.¸¸.• mahabat •.¸¸.••♥
Najua hautamani kusikia lolote kutoka kwangu kwa kuwa sina thamani tena kwako, thamani niliyokuwanayo kabla hujanipatia ujauzito mara mbili zote ukanisihi nitoe. Kwa sababu ninakupenda nilifanya yote unayotaka. Ulipodai kuwa ukitumia kondom hujisikii raha sikuogopa kuibeba mimba ya tatu nilikuambia fanya unavyotaka.
Nilifanya haya nikiamini kuwa nalinda penzi langu kwako!!!
Naumia sana leo unaponiita mimi Malaya!!! Mjinga tena mshamba!! Hakika hujakosea maana nilikuwa Malaya katika chumba chako, chumba ulichonifanya utakavyo tena kila siku, huku jukumu la kukisafisha ukiniachia mimi, kweli nilikuwa mjinga sana kwa kukulilia hata pale ulipokuwa umenikosea waziwazi na nilikuwa mshamba kwa kuwa ni wewe uliye nifundisha kufanya mapenzi kwa kutumia kila kiungo cha mwili wangu.

Babaa si unajua nilianza uhusiano na wewe maziwa yangu yakiwa wima, mbona leo wanifukuza ukidai kuwa hunitaki kwa kuwa nina maziwa makubwa tena yamelala. Hukumbuki ni wewe uliyeyafanya hivi???
Unaniita mimi mchafu sasa unasahau kuwa ni wewe u mchafu zaidi yangu, au unasahau jinsi ulivyokuwa mchafu kupitiliza, uchafu wako ulitokana tamaa zako za kimwili tamaa zilizokufanya ulitake penzi langu hata nilipokuwa katika siku zangu!!!!! Hukuwa ukiuona uchafu huu ati leo waniita mchafu!!!
Wewe una usafi gani???

Babaa!!! Nakuandikia haya japo utayapuuzia lakini unaujua ukweli kuwa nilikupenda na wala sio kimakosa. Nilifanya yote uliyoyataka lakini hunilipi thamani yangu tena leo hii.
Unazuga kuwa u wa mjini sana!!! Unasahau kuwa ulikuwa unakosa hata pesa ya nauli nikawa nakupatia akiba yangu ya pesa za pedi nilizokuwa nimepewa na mama.

Niliacha kulipa ada yangu nikakupatia pesa umnunulie mama yako dawa alipokuwa anaumwa, sijali sana hata kama ulinidanganya lakini nilifanya kwa mapenzi yangu kutoka moyoni.

Hivyo visichana vimekudanganyishia hayo mavazi yao kama viko uchi vile, macho yao ya wiziwizi yamekukamata unanisahau unasema ulipitiwa yaani ulinipenda bahati mbaya. Ulinipenda bahati mbaya???? Wakati ulikuwa unanililia, hivi kumbe machozi yako yalikuwa ya kunilaghai nashukuru umefanikiwa.
Lakini naomba nikwambie kitu kimoja babaangu, ulipoamua kujiingiza katika uhusiano na visichana vyako hivyo nilivumilia lakini siku nilipokufumania na yule rafiki yangu Jane mkifanya ngono makaburini niliumia sana, ni siku hiyo niliamua kujibu maombi ya yule rafiki yako Benard, siku hiyo nililala kwake, nilizini naye kwa hiari kwa lengo la kulipiza kisasi.
Kisasi kile hakikuyatuliza maumivu yangu, bado ulikuwa una nafasi katika moyo wangu!!!

Penzi lako halikuwa na mrithi baada ya siku mbili nilipata hamu ya kuwa na wewe nikaja kwako. Tukafanya mapenzi bila hata kukukumbushia juu ya uchafu ulionifanyia.
Nadhani lilikuwa kosa kubwa, kama ninavyokuandikia wewe barua hii usiyoipenda na mimi Benard aliniandikia na yeye aliandikiwa na Jane akadhani ni utani kumbe ni kweli tupu. Jane amethirika, amemwambukiza Bernard, Bernad kaniambukiza mimi halafu MIMI na JANE tumekuambukiza wewe.

Sikupenda iwe hivyo lakini na wewe sikulaumu!!!
Asante kwa kuisoma barua yangu, sina uhakika na maamuzi utakayochukua.
♥••.¸¸.• mahabat •.¸¸.••♥

No comments:

visitors comments