mmmmh


oo

Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

ningoje hadi lini

Mwenzio bado nangoja, ahadi uliyonipa,
Hali yangu reja reja, wala si ya kuchumpa,
Nilishazitowa hoja, basi sinitowe kapa,
Ningoje hadi lini?

Nambie lini wakati, utaponipa majibu,
Moyo kizungumkuti, kwani waupa adhabu,
Hauna tena ukuti, wakusubiri tabibu,
Ningoje hadi lini?

Kwamba nivute subira, nishasubiria sana,
Hadi hali yadorora, usiku nao mchana,
Nitoe kwenye madhara, nishazama kwacho kina,
Ningoje hadi lini?

Jibulo lanipa hamu, hamu ya kulisikia,
Ila sinipe wazimu, chonde sinipe umia,
Likoleze uhashamu, nifurahie dunia,
Ningoje hadi lini?

Usiku wote silali, wewe nakufikiria,
Mwenzio sinayo hali, jibu ninaliwazia,
Chonde mara mbili mbili, niepushie kulia,
Ningoje hadi lini?

Ninakonda ninakonda, nipo hoi taabani,
Chakula kinanishinda, hakinipiti kooni,
Fanya hima kunikanda, unondowe taabuni,
Ningoje hadi lini?

Nieleze yako nia, unondoe wasiwasi,
Nini unadhamiria, mana moyo wenda kasi,
Mwenzio nasubiria, chonde nijibu upesi,
Nimeshangoja sana.

visitors comments