mmmmh


oo

Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

mahanjumati btes

MKATE WA MAYAI
Mayai 6

Sukari kiasi cha vikombe vitatu vya kahawa

Unga wa ngano kiasi cha vikombe vitatu vya kahawa

Hiliki kiasi

Samli kidogo

Zabibu kiasi

Arki kidogo

♥*.¸¸.*♥
♥*.¸¸.*".:☻:."*.¸¸.*♥
*шєlςσмє*
♥*.¸¸.*".:☻:."*.¸¸.*♥
♥*.¸¸.*♥

to
)♦(
)♦( * )♦(
)♦(
:
`°(•´.¯`°`•.•´°´¯.`•)°´
mahanjumati webpage



Baking powder nusu kijiko cha chai

1 > Changanya unga mkavu na Baking Powder.

2 Chukua bakuli lenye nafasi utie sukari. Menya hiliki uzitwange. Kisha zichanganye na sukari na utie arki uipendayo. Vunja mayai yote utie. Chukua mchapo wa kupigia mayai uyapige mpaka yajae kiasi cha kutosha.

3 Chukua unga uwe unautia na huku unakoroga mpaka umalizike wote.

4 Chukua sufuria uipake samli iliyoganda pembezoni mote. Kisha mimina mayai yote ufunike. Upike mkate kwa moto wa mkaa, juu na chini. Angalia moto usiwe mkali sana. Utaunguza mkate. Moto uwe wa kiasi. Mkate ukianza kupiga wekundu chukua kujiti uuchome mpaka ndani. Ukiona kimetoka kikavu jua kuwa mkate umeshaiva. Uepue uache upoe. Baadae utoe kwa upole uweke kwenye sahani. Chukua zabibu tia ndani ya maji ya moto kidogo zipate kuregea. Baadae zipage juu ya mkate ukishaanza kupiga wekundu ndio uzitie.
*°•.¸¸.°mαhαηjumaτi βίtes ℓσαđiиg...°.

MKATE WA KUKAANGA KWA MAZIWA NA MAYAI


Maziwa ½ painti

Samli ¼ kilo

Mayai 3

Chumvi kiasi

Pilipili manga kiasi

Boflo 1 kubwa

1 Kata mkate wa boflo vipande vya kiasi. Piga mayai pamoja na chumvi kidogo na pilipili manga.

2 Teleka chuma utie samli. Ikianza kuchemka chukua vipande vya mkate uvichovye katika maziwa na baadae uvichovye katika mayai kisha uvitie katika chuma uvikaange. Vikiwa vimewiva upande mmoja geuza upande wa pili. Vikiwa tayari vitoe uvitie kwenye sahani.
*°•.¸¸.°mαhαηjumaτi βίtes ℓσαđiиg...°.

MKATE WA MAYAI NA JAM



Boflo kubwa 1

Mayai 4

Unga wa ngano kidogo

Jam kidogo

Samli ¼ kilo

1 Kata mkate vipande vyembamba vyembamba uvipake jam, kisha vigandanishe kimoja juu ya kingine.

2 Vunja mayai uyapige sana. kisha nyunyizia unga huku ukiendelea kuyapiga mayai.

3 Teleka chuma utie samli. Ikianza kuchemka vichovye vile vipande vya mkate ndani ya mayai na uvichome ndani ya samli. Vikiiva upande mmoja geuza upande wa pili kisha uvitoe uvitie kwenye sahani.
*°•.¸¸.°mαhαηjumaτi βίtes ℓσαđiиg...°.

MKATE WA NYAMA

Unga kilo 1

Nyama ¾ kilo

Vitunguu kilo 1

Samli ¾ kilo

Nazi nzuri 1

Thomu kiasi

Tangawizi mbichi kiasi

Pilipili manga kiasi

Limau kiasi

Chumvi kiasi

Hamira kiasi (inategemea hamira utakayoitumia)

1 Saga nyama uikoshe. Kata vitunguu vodogo vidogo kama vya sambusa. Menya thomu uitwange pamoja na tangawizi mbichi na pilipilimanga. Changanya nyama na vitunguu pamoja na viungo ulivyovitwanga utie chumvi na ukamulie limau, kisha uipike mpaka ikauke maji iwe kavu, halafu iipue uitandaze ipoe.

2 Kuna nazi uchuje tui zito. Chunga unga uvuruge kwa tui na chumvi na hamira halafu uweke uache uumuke. Unga usiwe mzito sana.

3 Teleka chuma utie samli kisha chota unga kwa vidole vyako utie juu ya chuma utandaze duara kiasi cha kitumbua, halafu chukua kijiko uteke nyama uitie juu ya ule unga uenee mote. Teka tena unga mwengine ufunike ile nyama yote kisha kisha uchukue kisu uusogeze katikati ya chuma ili uive vizuri. Uache uchemkie juu ya samli na huku ukiugeuzageuza upate kuiva vizuri. Pindua upande wa pili uuchome kama mwanzo mpaka uive. Unaweza kuchoma mikate miwili au mitatu kwa wakati mmoja. Choma mikate yote mpaka unga na nyama im
*°•.¸¸.°mαhαηjumaτi βίtes ℓσαđiиg...°.

VITUMBUA

Mchele kilo 1

Sukari ¼ kilo

Nazi kubwa 2

Hiliki kiasi

Hamira kiasi (inategemea hamira utakayoitumia)

Samli au mafuta ½ kilo

Mayai 4 (ukipenda)

1 Uroweke mchele uutwange uwe unga laini. Kuna nazi uchuje tui zito. Menya hiliki uitwange.

2 Changanya na sukari na hiliki, tia hamira na utie tui uvuruge uwe na wepesi wa kuweza kutekeka kwa upawa, halafu uache uumuke.

3 Teleka vijungu vidogo, ikiwa kimoja viwili au zaidi, kadri uwezavyo. Tia samli katika hivyo vijungu, ikichemka teka unga kwa upawa utie katika hivyo vijungu na baadae uufunike. Uache kwa muda kidogo viive halafu geuza upande wa pili kwa kutumia kijiti kilichotengenezwa vizuri ukiona upande wa pili umeshaiva vitoe. Endelea kuchoma hivi hivi mpaka wote umalizike. (Kila wakati mafuta au samli ikipingua unaongeza).
*°•.¸¸.°mαhαηjumaτi βίtes ℓσαđiиg...°.

VILOSA

Unga wa mchele kilo1

Sukari ¾ kilo

Samli kilo 1

Mtindi painti 1

Nazi 2 nzuri

Arki kiasi

Hiliki kiasi

Hamira kiasi

1 Kuna nazi uchuje tui zito. Menya hiliki uzitwange.

2 Changanya unga na sukari kidogo, hamira na mtindi, halafu uvuruge kwa tui hadi uwe mwepesi kuliko unga wa vitumbua. Uweke uumuke.

3 Tia maji kidogo katika sufuria utie na sukari, hiliki na arki upike shira nyepesi ya kiasi.

4 Unga ukishaumuka teleka vijungu kama vile vya kupika vitumbua utie samli. Ikichemka teka unga kwa upawa uanze kuvichoma vilosa. Tia unga katika vijungu kisha uvifunike. Wacha vitokote kwa muda mdogo kisha vitoe uviweke katika chujio vivuje mafuta, kisha vitumbukize katika shira. Endelea kuchoma mpaka vimalizike vyote.
*°•.¸¸.°mαhαηjumaτi βίtes ℓσαđiиg...°.

MAANDAZI

Unga kilo 1

Sukari ¼ kilo

Samli kilo 1

Nazi 1

Hamira kiasi

Hiliki kiasi

Arki kiasi

1 Kuna nazi uchuje tui zito.

2 Changanya unga, sukari, hiliki, arki na samli kidogo ukande kwa tui la nazi mpaka ulainike kisha uache uumuke.

3 Kata unga madonge ya kiasi usukume na ukate kwa namna upendayo.

4 Teleka karai juu ya moto utie samli. Ikichemka tia vipande vya unga uchome maandazi, yakiiva upande mmoja geuza upande wa pili. Endelea kuchoma mpaka umalize unga wote.
*°•.¸¸.°mαhαηjumaτi βίtes ℓσαđiиg...°.

MAANDAZI YA KIPEMBA

Unga kilo 1

Sukari ¼ kilo

Samli kidogo

Nazi 8

Hamira kiasi

Hiliki kiasi

Arki kiasi

Mayai 3

1 Kuna nazi uchuje tui zito. Menya hiliki uitwange.

2 Changanya unga, sukari, hiliki, arki, samli mayai na hamira ukande kwa tui la nazi mpaka uwe laini sana. Ukate unga madonge madonge halafu uusokote.Tafuta legeni lenye nafasi ulipakae samli. Uchukue ule unga uliokwisha sokota uuweke juu ya hilo legeni kwa nakshi uipendayo. Unaweza kufanya maandazi yenye nashi za aina mbali mbali. kisha uache uumuke.

3 Unga ukishaumuka usiutoe. Chukua sinia nyengine ufunikie juu yake na uyachome maandazi kwa kutia moto mdogo juu na chini.

4 Angalia, ukiona maandazi yameshaiva kwa kupiga wekundu yatoe uyaweke kwenye sahani.
*°•.¸¸.°mαhαηjumaτi βίtes ℓσαđiиg...°.

KALIMATI

Unga ¼ kilo

Samli ½ kilo

Sukari ½ kilo

Yai 1

Arki kiasi

Hamira kiasi

Hiliki kiasi

1 Changanya unga, samli kidogo, yai na hamira uvuruge kwa maji, usiwe mwepesi wala mzito sana. Uweke upate kuumuka.

2 Chukua hiliki uzimenye na kuzitwanga.

3 Teleka sufuria utie maji sukari, arki na hiliki uache ichemke mpaka iwe shira nyepesi.

4 Teleka karai utie samli. Ikianza kuchemka anza kuchoma kwa kuchota unga kwa vidole utie katika karai. Choma kaimati ndogo ndogo zenye umbo kama ndimu. Zichome kwa kuzigeuza geuza katika mafuta mpaka ziwe na rangi ya manjano. Zitoe uzitie katika chujio zivuje mafuta, kisha zitumbukize katika shira zipate kuingia shira ndani. Baadae zitoe uziweke kwenye sahani.
*°•.¸¸.°mαhαηjumaτi βίtes ℓσαđiиg...°.

MKATE WA NYAMA

Nyama ½ kilo

Vitunguu maji ½ kilo

Samli ½ kilo

Unga ¼ kilo mayai 4

Pilipili manga kiasi

Bizari nzima kiasi

Tangawizi mbichi kiasi

Vitunguu thomu kiasi

Baking Powder ½ kijiko cha chai

Limao kiasi

Chumvi kiasi

1 Osha nyama iliyokwisha sagwa uichuje maji yote. Menya vitunguu uvioshe uvikate vidogo vidogo kama vya sambusa. Menya vitunguu thomu usage pamoja na tangawizi mbichi. Twanga pilipilimanga pamoja na bizari nzima.

2 Changanya nyama na vitunguu pamoja na viungo vyote ulivyovisaga na kuvitwanga, tia chumvi na limau. Ipike nyama pamoja na viungo vyote mpaka ikauke. Epua uitandaze ipoe.

3 Chunga unga uufikiche kwa samli iliyoyeyushwa utie Baking Powder uukande kwa maji yaliyotiwa chumvi kidogo mpaka ulainike. Ukate unga madonge mawili. Tia unga mkavu juu ya kibao cha kusukumia, usukume uenee kibao chote. Vunja yai moja ulitie katikati ya unga uliousukuma ulitandaze. Chukua nyama utie juu ya lile yai na uitandaze ikae pembe nne, kiasi cha inchi 6 kila upande. Vunja yai la pili juu ya nyama na baadae ufunike kwa ule unga uliobakia pembeni kama bahasha ya pembe nne. Fanya mkate wa pili kwa vitu vilivyobakia kama wa kwanza. (Kwa sababu vipimo tulivyotoa ni vya mikate miwili).

4 Teleka chuma juu ya moto utie samli. Ikipata moto tia mkate uuchome kwa utaratibu, hautaki moto mkali ukishaiva upande wa kwanza geuza upande wa pili na ukiiva utoe uchome wa pili hivyo hivyo.
*°•.¸¸.°mαhαηjumaτi βίtes ℓσαđiиg...°.

No comments:

visitors comments