mmmmh


oo

Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

wazo la leo

japo maisha popote lakini huwezi kuishi
chooni
...........................
Hata uwe na magari millioni chooni lazima utaenda kwa miguu.
.........................
vitungu ,nyanya , carot navyo ni
viungo lakini havipangwi kwenye match.
...........................
usiteme Big G kwa karanga za kuonjeshwa
Usiache mbachao kwa msala upitao
......................
Kulia na kucheka zote ni kelele!
..........................
mlango wa gunia hauwekwi komeo...
..........................
Kama kutoa ni moyo basi kujumlisha ni figo.
...........................
UKISIKIA KITUO CHA POLISI KINAUZWA NIJULISHE
................................
hata uwe na mdomo mkubwa vipi huwezi
kuimba kwaya peke yako
............................
Kiwembe nacho kinakata ila hakina diwani.!!
.............................
Hata uwe na habari nzito kiasi gani
huwezi omba mtu akutwishe..!
..........................
Hata habari ziwe moto moto kiasi gani
haziwezi kuunguza gazeti.
....................
taa kila siku inawashwa lakini nashangaa haijikuni
...........................
Kumbuka Rushwa haina risiti..!!
........................
Mtindi nao unaganda lakini haumenywi kabla ya kula..!!
...........................
Kama mtoto mdogo ni MCHANGA basi mtu mzima ni SEMENTI
.........................
Na hata uwe na vurugu vipi wakati wa kujisaidi lazima utulie
...........................
Hata Mti unaota ingawa haulali usingizi....!!
..............................
Dobi nae ni mpiga pasi hodari
lakini kamwe hasikiki kwenye klabu za soka
...........................
WAZO LA FASTAFASTA: Heshima pesa shikamoo makelele
.......................
hata draft lina vyumba lakini havipangishwi..!!
........................
Na vile vile kukaa karibu na mahakama sio kujua sheria
..............................
Kuku nae ni ndege sema tu hatui Aiport
.......................
WAZO LA CHAPCHAP: Japo jogoo anawahi kumka hawezi fungua mlango.
......................
Hata Pundamilia ana mistari, sema tu hana mkwanja wa kuingia studio
.........................
Ujinga ni kuifanyia lamination ATM card.
..........................
Ebwana hata kama unapenda kuonja namna gani. Huwezi onja maji ya ugali
..........................
Mwanamke tabia, sura hata mbuzi anayo
..........................
Hata uwe DJ mkali namna gani huwezi piga wimbo wa taifa disco
..............................
Lakini kumbuka, hata ujue kuendesha gari kiasi gani,
tumbo la kuhara halina leseni.
............................
Kumbuka unaweza shika kila kitu
 lakini huwezi kuishika adabu..!!
..........................
serikali itapandisha kila kitu
 lakini haiwezi kupandisha mashetani
............................
kusoma kuelewa kufaulu matokeo
...........................
Tumia kichwa kufikiria siyo
 kufugia nywele pekee
.........................
gunia tupu halisimami
......................
"Hata chupi ichakae vipi huwezi kufanya dekio"
..........................
"Na hata uwe na haraka kiasi gani
 huwezi funga supu kwa gazeti
.........................
Lakini kumbuka hata uwe
kinyozi hodari kiasi gani,
 huwezi nyoa kichwa cha habari.
.......................
Daah kutembea kwangu kote
 sijaona mwanajeshi zeruzeru!!
............................
Hata uwe dereva kiasi gani huwezi
piga norinda treni.
.........................
Lakini kumbuka: Utaosha vyombo
vyote,lakini huwezi kuosha vyombo
 vya habari
..........................
Kumpiga chura teke ni kumuongezea mwendo
..........................
Read More ->>

No comments:

visitors comments