mmmmh


oo

Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

white house romance

Kipindi cha maswali na majibu kilimalizika katika kikao hiki cha nane cha mkutano wa nne wa bunge

la jamhuri ya muungano wa Tanzania.Maswali yote yaliyopangwa kuulizwa siku hii yalipata nafasi na

majibu muafaka toka kwa mawaziri husika.Kumalizika kwa maswali kukampa spika wa bunge Bi

Bernadetha makawala nafasi ya kusimama na kusema machache ikiwa ni pamoja na kutambulisha wageni

muhimu na kusoma matangazo mbali mbali ya kazi .WHITE HOUSE ROMANCE

Dakika takribani tano alizitumia katika kusoma matangazo ya kazi na kuwatambulisha baadhi tu ya

wageni waliohudhuria kikao hiki,halafu akamwita katibu wa shughuli za bunge siku hiyo ndugu Wilson

ndendeki aweze kuliongoza bunge kwa shughuli inayofuata.Akasimama na kutamka shughuli inayofuata
“Hoja binafsi za wabunge”
Baada ya kauli hiyo spika wa bunge akasimama na kutoa maelekezo mafupi.
“Waheshimiwa wabunge ,leo tutakuwa na hoja binafsi mbili.Ya kwanza inatoka kwa mheshimiwa mbunge

Romana salvatory inayohusu kufilisika kwa benki ya taifa ya vijana .Hoja ya pili inatoka kwa

mheshimiwa mbunge Marewa shawe inahusu uvunaji wa mazao ya misitu katika msitu wa Isambe..Kila

mtoa hoja amepewa muda usiozidi dakika sitini za kuwasilisha hoja yake.Kwa kuwa hatutakuwa na muda

wa kutosha wa kuanza kuzichangia hoja hii katika kipindi hiki cha asubuhi basi tutakaporudi mchana

tutaanza moja kwa moja kuchangia katika hoja zote mbili kwa pamoja.Kwa maana hiyo mnatakiwa muanze

kujiorodhesha kuchangia hoja hizi kuanzia sasa hivi ili tuone tutakuwa na wachangiaji wangapi

mpaka mchana.Naomba sasa nimwite mtoa hoja wa kwanza mheshimiwa Romana salvatory.Karibu sana

mheshimiwa” Spika akakaa katika kiti chake tayari kwa kuanza kuisikiliza hoja ya mheshimiwa

mbunge Romana mmoja kati ya wabunge vijana machachari mno .
Bunge lote lilikuwa kimya kabisa wakimsubiri mhesimiwa mbunge ainuke.Mheshimiwa Romana alikuwa

ameinamia meza yake bila kustuka hali inayomlazimu spika kusimama tena.
“Mheshimiwa mbunge ,tafadhali karibu uwasilishe hoja yako.”
Pamoja na mwito ule wa spika bado mheshimiwa mbunge alikuwa ameinamia meza yake.Wabunge wote

wakageuza vichwa vyao kumuangalia mheshimiwa mbunge yule kijana huku wengine wakidhani labda

amepitiwa na usingizi.Minong’ono na vicheko vya chini chini vikaanza kusikika..Spika akasema
“Waheshimiwa wabunge mlio karibu naye hebu tusaidieni kumstua hapo “
Mheshimiwa Salama awadh mbunge wa viti maalum akainuka na kwenda kumstua.Akamshika bega na

kumtikisa kidogo,lakini bado mheshimiwa mbunge hakuamka,akampiga piga mgongoni lakini bado

hakuonyesha dalili zozote za kustuka ndipo alipoamua kumuinua kichwa.Nusura aanguke kwa mstuko

alioupata.Mheshimiwa mbunge Roma alikuwa hana fahamu,jasho linamtiririka usoni na povu

mdomoni.Bunge lote linakumbwa na taharuki.Haraka haraka wabunge waliokuwa karibu wakamuinua na

kumtoa nje kumkimbiza katika zahanati ya bunge.Shughuli za bunge zikasimama kwa muda.Ni muda

mchache tu uliopita mheshimiwa mbunge Roma alikuwa mzima wa afya na alipata nafasi ya kuuliza

swali la nyongeza katika kipindi cha maswali na majibu,hakuonyesha dalili zozote za ugonjwa.Hali

iliyomtokea ilimpa wasi wasi kila mtu mle bungeni.
“Waheshimiwa wabunge naomba tukae…..” Ilikuwa ni sauti ya mheshimiwa spika akiwataka wabunge

watulie na shughuli za bunge ziweze kuendelea.Bado mazungumzo yaliendelea licha ya mwito ule wa

spika.
“Naomba utulivu ndani ya bunge tafadhali….waheshimiwa wabunge naomba tukae katika sehemu zetu ili

shughuli za bunge ziweze kuendelea.”
Taratibu wabunge wakaanza kurejea katika sehemu zao na mazungumzo yakapungua.
“Waheshimiwa wabunge,mwenzetu amepatwa na matatizo ya ghafla na amepelekwa katika zahanati yetu

ya bunge kwa huduma ya kwanza.Naomba tuwe watulivu wakati mwenzetu anapatiwa matibabu.Mtajulishwa

kila kitu juu ya maendeleleo yake baada ya uchunguzi wa kidaktari kufanyika.Kwa sasa naomba

shughuli za bunge ziendelee.Kwa kuwa mheshimiwa Roma ndiye aliyekuwa awe wa kwanza kuwasilisha

hoja yake asubuhi hii napenda sasa nimwite mheshimiwa Marewa aweze kuwasilisha hoja yake.Hoja ya

mheshimiwa Roma tutaipangia siku nyingine.Mheshimiwa marewa karibu uwasilishe hoja yako”
****************************************************************
Zahanati ya bunge ghafla ikageuka sehemu ya heka heka .Madaktari wa bunge walikuwa wakijitahidi

kwa kila walivyoweza kumpa huduma ya kwanza mheshimiwa Roma .Vipimo vya awali vilionyesha kuwa

shinikizo la damu lilikuwa juu isivyo kawaida na hata sukari ilikuwa imepanda mno.Pamoja na

jitihada zote za madaktari wa bunge bado hali ya mheshimiwa mbunge iliendelea kuwa mbaya

,ikamlazimu daktari mkuu wa bunge aamuru mheshimiwa spika aitwe.
Akiwa mezani kwake huku mheshimiwa mbunge Marewa shawe akiendelea kuwasilisha hoja yake,mhudumu

wa bunge akampelekea ujumbe wa kumtaka afike mara moja katika zahanati ya bunge.Bila kupoteza hata

sekunde spika akasimama na mheshimiwa aliyekuwa akiendelea kuwasilisha hoja yake akanyamaza

kumpisha spika wa bunge.
“waheshimiwa wabunge,nimepata taarifa toka kwa daktari wetu mkuu wa bunge akinitaka nifike mara

moja katika zahanati yetu.Naomba nimuachie naibu spika aweze kuendelea na shughuli zilizobaki za

bunge.”
Kitu cha kwanza alichotaka kufahamu mheshimiwa spika baada ya kufika katika zahanati ya bunge ni

hali ya mheshimiwa Roma.Daktari akamuomba waongozane hadi katika ofisi yake.
“Daktari hebu nieleze hali ya mbunge inaendeleaje? Anasumbuliwa na kitu gani? Akauliza mheshimiwa

spika .
“Mheshimiwa spika nimeona nikuite nikueleze ukweli kwamba hali ya mbunge si nzuri hata

kidogo.Vipimo vyetu vinaonyesha kuwa shinikizo la damu liko juu mno na hata sukari yake imepanda

sana.Mpaka sasa hivi bado hatujaweza kufanikiwa kushusha sukari wala shinikizo la damu.Hali ya

mbunge inaendelea kwa mbaya hivyo nashauri haraka sana tumuwahishe katika hospitali kuu ya St

Francis ili akachekiwe zaidi.”
Huku uso wake ukionyesha wasi wasi mheshimiwa spika akaamuru haraka sana mheshimiwa Roma

ahamishiwe katika hospitali ya St Francis.Ni kitendo ambacho hakikuchukua hata dakika kumi tayari

mbunge alikwisha pakiwa katika gari la wagonjwa na kukimbizwa St Francis hospital.
Madaktari na wauguzi walikuwa wamekwisha jiandaa kumpokea mheshimiwa mbunge.Walikwisha pigiwa

simu na ofisi ya bunge.Baada tu ya gari kusimama kitanda kinashushwa na mheshimiwa mbunge

akakimbizwa katika chumba cha wagonjwa mahututi.Mara moja mheshimiwa Roma akaanza kupatiwa

matibabu.Kwa zaidi ya nusu saa juhudi zikaendelea za kuhakikisha hali ya mheshimiwa huyu kijana

kipenzi cha wengi inaimarika lakini bado hali yake ikaendelea kuwa mbaya na kuwashangaza hata

madaktari.Mwishowe madaktari wakafikia uamuzi wa kumuhamishia mheshimiwa Roma katika hospitali kuu

ya magonjwa ya moyo Tanzania Heart hospital iliyoko jijini Dar es salaam.

Zahanati ya bunge ghafla ikageuka sehemu ya heka heka .Madaktari wa bunge walikuwa wakijitahidi

kwa kila walivyoweza kumpa huduma ya kwanza mheshimiwa Roma .Vipimo vya awali vilionyesha kuwa

shinikizo la damu lilikuwa juu isivyo kawaida na hata sukari ilikuwa imepanda mno.Pamoja na

jitihada zote za madaktari wa bunge bado hali ya mheshimiwa mbunge iliendelea kuwa mbaya

,ikamlazimu daktari mkuu wa bunge aamuru mheshimiwa spika aitwe.
Akiwa mezani kwake huku mheshimiwa mbunge Marewa shawe akiendelea kuwasilisha hoja yake,mhudumu

wa bunge akampelekea ujumbe wa kumtaka afike mara moja katika zahanati ya bunge.Bila kupoteza hata

sekunde spika akasimama na mheshimiwa aliyekuwa akiendelea kuwasilisha hoja yake akanyamaza

kumpisha spika wa bunge.
“waheshimiwa wabunge,nimepata taarifa toka kwa daktari wetu mkuu wa bunge akinitaka nifike mara

moja katika zahanati yetu.Naomba nimuachie naibu spika aweze kuendelea na shughuli zilizobaki za

bunge.”
Kitu cha kwanza alichotaka kufahamu mheshimiwa spika baada ya kufika katika zahanati ya bunge ni

hali ya mheshimiwa Roma.Daktari akamuomba waongozane hadi katika ofisi yake.
“Daktari hebu nieleze hali ya mbunge inaendeleaje? Anasumbuliwa na kitu gani? Akauliza mheshimiwa

spika .
“Mheshimiwa spika nimeona nikuite nikueleze ukweli kwamba hali ya mbunge si nzuri hata

kidogo.Vipimo vyetu vinaonyesha kuwa shinikizo la damu liko juu mno na hata sukari yake imepanda

sana.Mpaka sasa hivi bado hatujaweza kufanikiwa kushusha sukari wala shinikizo la damu.Hali ya

mbunge inaendelea kwa mbaya hivyo nashauri haraka sana tumuwahishe katika hospitali kuu ya St

Francis ili akachekiwe zaidi.”
Huku uso wake ukionyesha wasi wasi mheshimiwa spika akaamuru haraka sana mheshimiwa Roma

ahamishiwe katika hospitali ya St Francis.Ni kitendo ambacho hakikuchukua hata dakika kumi tayari

mbunge alikwisha pakiwa katika gari la wagonjwa na kukimbizwa St Francis hospital.
Madaktari na wauguzi walikuwa wamekwisha jiandaa kumpokea mheshimiwa mbunge.Walikwisha pigiwa

simu na ofisi ya bunge.Baada tu ya gari kusimama kitanda kinashushwa na mheshimiwa mbunge

akakimbizwa katika chumba cha wagonjwa mahututi.Mara moja mheshimiwa Roma akaanza kupatiwa

matibabu.Kwa zaidi ya nusu saa juhudi zikaendelea za kuhakikisha hali ya mheshimiwa huyu kijana

kipenzi cha wengi inaimarika lakini bado hali yake ikaendelea kuwa mbaya na kuwashangaza hata

madaktari.Mwishowe madaktari wakafikia uamuzi wa kumuhamishia mheshimiwa Roma katika hospitali kuu

ya magonjwa ya moyo Tanzania Heart hospital iliyoko jijini Dar es salaam.
*******************************************************
Kupitia matangazo ya moja kwa moja yaliyokuwa ywakirushwa na vituo mbali mbali vya televisheni na

hata redio Taifa zima liliweza kushuhudia na kusikia moja kwa moja kilichotokea bungeni.Uikuwa ni

mstuko mkubwa sana.Kutokana na ukuaji wa teknolojia,ka kipindi kifupi sana idadi kubwa ya watu

waliweza kupata taarifa ya kilichojiri bungeni. Kupitia mitandao ya kijamii,simu za mikononi,blogs

na vyombo vingine vya upashanaji habari taarifa ziliweza kuwafikia watu kwa haraka mno.Taarifa

kubwa iliyokuwa ikizunguka katika mitandano na jumbe za simu za mikononi ni kwamba Mheshimiwa Roma

amefariki dunia ghafla.Taarifa hii ilisababisha shughuli ziweze kusimama kwa muda.Taifa

likazizima.Watu wengi walikuwa na mapenzi makubwa kwa mbunge huyu kijana.Mheshimiwa Roma alipendwa

na watu wa rika zote bila kujali itikadi ya dini au vyama.Kuanzia shule za msingi hadi vyuo

vikuu,toka kwa muuza nyaya Kariakoo hadi kwa mkulima wa korosho kule Mtwara,toka kwa mvuvi wa

samaki Kigoma hadi kwa mfugaji ngorongoro.Wengi walikuwa na imani kuwa muda utakapofika basi huyu

ndiye angeweza kuwa raisi wa Tanzania na kuwakomboa watanzania katika maisha duni waliyokuwa

nayo.Hii ilitokana na uzalendo wa kweli aliouonyesha kijana huyu katka kipindi kifupi.
Taarifa zikaanza kusambaa tena kuwa mwili wa mheshimiwa Roma ulikuwa njiani kusafirishwa kwa

ndege kuja Dar es salaam.Makundi ya vijana yakaanza kukimbia kuelekea uwanja wa ndege wa Dar es

laam ili kuweza kuhakikisha kama taarifa hizi ni za kweli.
“Hatuwezi kukubali wametuulia raisi wetu….” Alisema kwa jazaba kijana mmoja aliyekuwa akikimbia

huku amevua shati na jasho likimtiririka mwili mzima akielekea uwanja wa ndege.
Kundi jingine la vijana watembeza bidhaa barabarani maarufu kama machinga lililokuwa na vijana

wapatao mia moja na zaidi nalo lilikuwa lilikimbia kuelekea uwanja wa ndege ilimradi kila mmoja

aliyeguswa na taarifa ile ya kustusha alitaka kuhakikisha kwa macho yake mwenyewe .
***********************************************************
Ndege iliyombeba mheshimiwa Roma ilitua katika uwanja wa kimataifa wa Julius Nyerere.Kwa

haraka mgonjwa akashushwa nakupakiwa katika gari la wagonjwa na kukimbizwa katika hospitali kuu ya

magonjwa ya moyo Tanzania heart hospital.Waandishi wengi wa habari na wapiga picha walikuwa

wamejazana hapo uwanjani ili kuweza kujaribu kupata walau habari na picha za tukio hili ili kuweza

kuuhabarisha umma wa watanzania uliokuwa ukisubiri taarifa zenye uhakika kwa hamu kubwa.Kwa jinsi

ulinzi ulivyokuwa umeimarishwa na kwa tukio lenyewe lilivyokuwa la haraka ilikuwa ngumu kuweza

kuipata picha ya moja kwa moja ya mheshimiwa mbunge.Picha zilipigwa kwa kutumia kamera zenye nguvu

zenye kuweza kunasa tukio katika umbali mrefu.
Gari la wagonjwa likiwa limetanguliwa na piki piki ya polisi liliondoka kwa kasi hapo

uwanjani na kuwaacha watu wakiwa kimya na wengine wakiangua vilio wakijua ni kweli mpendwa wao

mheshimiwa Roma alikuwa amefariki dunia.
Tanzania heart hospital hospitali binafsi inayomilikiwa na daktari bingwa wa magonjwa ya moyo

Dr Sandra Jeremy mpama,mtoto wa rais wa jamhuri ya muungano Tanzania ,ilikwisha taarifiwa juu ya

kuletwa kwa mheshimiwa mbunge hivyo madaktari na wauguzi waliwekwa tayari ili pindi tu mgonjwa

atakapofika basi aanze kushughulikiwa haraka iwezekanavyo..Hopsitali hii ni moja kati ya hospitali

kubwa ya magonjwa ya moyo katika ukanda huu wa afrika mashariki,iliyosheheni madaktari bingwa wa

moyo.Japo ni hospitali binafsi lakini inatumika kama hospitali ya rufaa kwa watu wennye maradhi ya

moyo.
Geti linafunguliwa na kuiruhusu piki piki ya polisi iliyoliongoza gari la wagonjwa lililombeba

mheshimiwa Roma kupita .Baada tu ya kusimama ,mheshimiwa akashushwa na kukimbizwa katika katika

chumba maalum cha wagonjwa mahututi.Kazi ya kumuhudumia ikaanza.
**************************************************************
Umati wa watu ulizidi kuongezeka katika kila dadkika.Hakuna aliyeruhusiwa kuingia ndani

hospitalini zaidi ya viongozi wachache wa serikali ambao hata nao hawakuweza kumuona mheshimiwa

Roma kwa sababu bado alikuwa akiendelea kupata matibabu katika chumba cha wagonjwa mahututi.Watu

walikaa nje ya jengo la hospitali wakiongozwa na waandishi wa habari waliokuwa wakijitahidi kwa

kila namna ili kuweza kupata taarifa za nini kilichokuwa kikiendelea mle ndani. Mpaka saa kumi

na moja za jioni bado hakukuwa na taarifa zozote toka ndani ya hospitali juu ya maendeleo ya

mgonjwa.Yapata saa kumi na mbili za jioni mheshimiwa spika wa bunge akawasili ,akafunguliwa geti

na kuingia ndani.Akiwa ameongozana na baadhi ya wabunge na maofisa wengine wa bunge waliweza

kuingia hospitalini hapo lakini taarifa aliyopewa ni kwamba bado hali ya mheshimiwa mbunge haikuwa

nzuri..Spika na ujumbe wake wakatoka humo hospitali na kuondoka kwa sababu hakukuwa na ulazima wa

wao kuendelea kuwepo hapo hospitali wakati bado mgonjwa alikuwa akipatiwa matibabu.
****************************************************************
WHITE HORSE HOTEL - DODOMA
“Na sasa tugonganishe glasi zetu kusherehekea ushindi mkubwa tulioupata.” Kila mmoja akainua glasi

yake ya mvinyo na glasi zikagonganishwa.
Ni katika hoteli tulivu ya white horse hoteli,hoteli yenye hadhi ya nyota tano ambayo ni baadhi

tu ya vigogo ndio huwa wanafikia hapa,katika chumba kikubwa chenye hadhi ya presidential suit

kilichopangwa na Mr Faidh al badir,mmoja kati ya wafanya biashara wakubwa sana nchini akiwa na

wabunge watatu wa bunge la jamburi ya muungano wa Tanzania na watu wengine wawili ,walikuwa

wakijipongeza.
“Mr Nkebo nimeamini wewe ni mtu hatari sana.Unajua bila wewe leo hii huyu kijana alikuwa

atuaibishe vibaya mno.Lengo lake lilikuwa kuutangazia umma kuwa sisi ndio tulioshiriki katika

kuifilisi ile benki ya Taifa ya vijana Tanzania.Lakini sasa kwisha habari yake…Na hili ni fundisho

kwake kuwa siku nyingine asijaribu kufuatilia mambo yasiyomuhusu” Ilikuwa ni kauli ya mheshimiwa

mbunge Nasoro ngimarwa.
“hahahahaaa….mimi ndio Nkebo bwana.Yule kijana mdogo sana hawezi kusindana na watu kama

sisi.Nilikwisha waambia kuwa msiwe na wasi wasi hata kidogo.Huu mswaada binafsi hauwezi

somwa.Najua wengine hamkuamini kabisa niliyokuwa nawaambia.Kwa wale ambao hamkuwa mkijua

kilichokuwa kikiendelea ni kwamba mheshimiwa Ngimarwa hapa alipata taarifa ya kuwapo kwa nia ya

kuwasilishwa hoja binafsi bungeni na mheshimiwa Roma juu ya kufilisika kwa benki ya vijana.Baada

ya utafiti tuligundua kuwa yule kijana tayari alikuwa na baadhi ya taarifa zinazotuhusisha sisi na

kufilisika kwa bennki ile na hata baadhi ya nyaraka ambazo zingeweza kutuweka sisi matatani

alikuwa nazo.Kitu cha kwanza kilichofanyika ni kupoteza ushahidi wote Ili hata kama lingetokea

pendekezo la kuundwa kwa kamati teule ya bunge kuchunguza sakata hili wasingeweza kutuhusisha

kabisa sisi na suala hili.Hilo lilifanikiwa .Pamoja na kufanikiwa huko bado kijana yule aliendelea

kuonekana hatari kwetu.Alikwisha tujua na hivyo asingeweza kuacha kutuandama.Nadhani mnajua jinsi

ambavyo anaungwa mkono na wananchi.Baada ya kuliona hilo tukaamua kuwa sasa kilichobaki ni kumuua

tu.Mpango ulianza kusukwa toka mkutano wa bunge uliopita.Tukagundua kuwa kijana yule anapenda

kufikia HD LODGE.Basi pale tukampatia kazi binti ambaye ndiye aliyeweza kumaliza mchezo wote wa

leo.Binti huyu ndiye aliyepangiwa kumuhudimia yule kijana na ndiye aliyeweka sabuni ambayo Roma

amaeogea leo.Sabuni hiyo ilikuwa na sumu kali ambayo hupenya na kuingia mwilini haraka sana mara

tu inapopakwa katika ngozi na kwa kawaida hii hufanya kazi taratibu na baada ya masaa manne toka

iingie mwili basi mgonjwa anaweza kufa.Kilichomuweka hai mpaka sasa hivi ni hizi dawa alizopewa

katika hositali ya St francis.Hizi zimechangia kumuweka hai mpaka sasa hivi.Lakini nawahakikishia

kuwa mheshimiwa huyu hawezi kufika asubuhi.Hata wafanye nini ni lazima atakufa tu.”
Wote wakampongeza Mr Nkebo kwa kazi kubwa na nzuri aliyoifanya.Wakaendelea kujimiminia mvinyo

katika maglasi na kunywa kwa furaha na kutakiana maisha marefu.
*******************************************************************
Saa mbili za usiku ,katika hospitali alimokuwa amelazwa mheshimiwa Roma,Daktari bingwa wa magonjwa

ya moyo Dr Sandra Jeremy Mpama akajitokeza mbele ya waandishi wa habari waliokuwa wamekusanywa

katika chumba cha mikutano cha hospitali hiyo.Akakaa kitini na chumba chote kikawa kimya kabisa.
“Ndugu wandishi wa habari nimewaiteni hapa ili kuwapa taarifa fupi juu ya mgonjwa tuliyempokea

hapa leo mheshimiwa Roma .Taarifa ninayotaka kuwapa si nzuri....................................
“Leo mchana tumempokea mheshimiwa mbunge Roma akisumbuliwa na shinikizo la damu.Toka tumempokea

tumekuwa tukijitahidi kwa kila tuwezalo ili kuhakikisha kuwa mwenendo wa mzunguko wa damu mwilini

unakuwa wa kawaida lakini napenda kusema kuwa bado hali ya mbunge si nzuri.Napenda kuchukua nafasi

hii kukanusha uvumi ulioenea na unaoendelea kuenea kuwa mheshimia Roma amefariki dunia.Taarifa ya

ukweli ni kwamba mheshimiwa mbunge ni mzima japo hali yake si nzuri lakini napenda niwatoe hofu

watanzania kuwa mbunge wetu atapona kwa sababu anashughulikiwa na timu yetu nzima ya madaktari

bingwa wa moyo wakiongozwa na mimi mwenyewe.Narudia tena kuwatoa hofu watanzania kuwa mbunge wetu

ni mzima na anaendelea kupata matibabu.Kinachotakiwa ni kuzidi kumuombea ili Mweneyzi Mungu ampe

uponaji wa haraka.Ahsanteni.
Akamaliza Dr Sandra ,akainuka na kutoka humo ukumbini huku waandishi wa habari wakisimama kutaka

kuuliza maswali.
“Jamani Dokta hana muda wa kujibu maswali yenu.Bado wanaendelea na kazi.Subirini kwanza wamalize

kazo zao ndio mtapata muda mzuri wa kumuuliza maswali yenu”
Dr Kalufa akawaambia wandishi wa habari.
Alipotoka kuzunguma na waandishi wa habari ,Dr Sandra akarudi tena katika chumba cha uangalizi

maalum kuungana na madaktari wenzake.Bado hali ya mheshimiwa Roma haikuonyesha dalili zozote za

matumaini.Hili lilimuumza mno Dr Sandra.Akatoka na kwenda ofisini kwake akakaa kitini huku

akitafakari nini cha kufanya.Ugonjwa huu ulimshangaza mno.Baada ya kama dakika tano za tafakaroi

akachukua simu na kumpigia msaidizi wake.
“Susan ,naomba mtaarifu Spika wa bunge kuwa namuhitaji haraka hapa hospitali”
Muda wa dakika ishirini toka apate mwito ule wa haraka spika wa bunge akawasili

hospitali.Akapokelewa na moja kwa moja akapelekwa katika ofisi ya Dr Sandra.
“Mheshimiwa Spika,naomba kwanza nikuombe samahani kwa mwito huu wa haraka” akaanza maongezi Dr

Sandra
“Usijali Dr Sandra.Hii ni moja ya majukumu yangu ya kazi kuhakikisha wabunge wote wanapopatwa

na hali kama hii kupata matibabu na kupona.Nimeacha vikao vya bunge vikiendelea ili kuja

kuhakiksha kuwa mheshimiwa mbunge anapata tiba stahili kwa sababu ugonjwa wake umetustua mno.Vipi

maendeleo yake kwa sasa?
“Mheshimiwa Spika napenda niwe wazi kuwa tumejitahidi sana toka tulipompokea hapa mchana lakini

bado hali yake haionyeshi mabadiliko .Bado tunaendelea na uchunguzi wa nini kinachosababisha hali

hii.Mheshimiwa spika hospitali yetu ni kubwa na ya kuaminika katika ukanda huu wa afrika mashariki

na kati na imesheheni madaktari bingwa wa magonjwa ya moyo.Pamoja na ukubwa na sifa hizo zote

tulizonazo napenda nitoe pendekezo kuwa mheshimiwa mbunge anahitaji kupelekwa nje ya nchi haraka

iwezekanavyo kwa matibabu zaidi.Mimi ni daktari bingwa wa moyo lakini kwa ugonjwa huu ninavyouona

hatuna njia nyingine zaidi a kumpeleka mgonjwa katika hospitali kubwa zaidi kwa uchunguzi

mpana.Kuna hospitali moja iko nchini Israel katika mji wa Haifa inaitwa Rambam medical center.Pale

wamesheheni mabingwa wa moyo na kuna vifaa vikubwa zaidi vya uchunguzi kuliko tuliyo navyo

sisi.Hospitali hii ni rafiki zetu na tumekuwa tukisaidiana mara kwa mara na hata kubadilishana

wataalamu.Nimekwisha ongea nao na wako tayari kumpokea mheshimiwa na kumsaidia”
Dr Sandra akamaliza na kumtazama Mheshimiwa Spika aliyekuwa amenyamaza akimsikiliza kwa makini

sana.Akainama kidogo akafikiri kisha akasema.
“Dr Sandra nakushukuru sana kwa jitihada zote unazozichukua kuhakikisha kuwa mbunge wetu

anapona.Mimi huyu mbunge ninamlea kama mwanangu Licha ya kwamba mimi ndiye kiongozi wake bungeni

lakni kama mzazi na kama mtanzania mwenye moyo wa uzalendo niko tayari kwa lolote lile linaloweza

kufanyika litakalomsaidia kijana huyu apone.Tatizo lililoko hapa Dr Sandra ni kwamba kuna taratibu

za kisheria ambazo ni lazima zifuatwe.Ingekuwa ni kwa ridhaa yangu basi ningekuruhusu sasa hivi

umuandae mgonjwa kwa safari.Kwa kuwa umeshauri hivyo ngoja na mimi nimpigie simu waziri wa afya

ambaye yuko hapa hapa Dar ili tukutane usiku huu huu na kuona nini cha kufanya.Yeye ndiye mwenye

dhamana ya kuamua nani na nani wapelekwe nje ya nchi kwa matibabu.”
Dr Sandra akamtazama Spika kwa makini sana kisha akasema kwa sauti ya taratibu.
“Nalifahamu hilo mheshimiwa Spika ,lakini kwa leo sidhani kama utaratibu huo una

nafasi.Kinachotakiwa hapa si utaratibu bali maamuzi ya haraka.Iwapo mtaanza kuvutana kuhusu

utaratibu kuna hatari ya kumpoteza mgonjwa.”
“Dr Sandra mambo ya kiserikali ni magumu .Siwezi kutoa uamuzi mimi mwenyewe hapa bila kufuata

taratibu husika.Ninachoomba nipe kama saa moja hivi iliniweze kukutana na waziri wa afya na tuone

tulifanyaje suala hili.”


Spika wa bunge akatoka ofisini kwa Dr Sandra kwa kasi.
Dr maneno kilugwa ,waziri wa afya katika serikali ya jamburi ya muungano wa Tanzania alikuwa

amejipumzisha katika mgahawa tulivu katika ufukwe wa bahari.Ni siku ya mwisho ya mkutano wa wadau

wa afya afrika,mkutano uliochukua takribani siku nne na uliomfanya asiwepo Dodoma katika vikao vya

bunge.Baada ya kazi ngumu iliyofanyika ya kuhakikisha kuwa mkutano ule unafanikiwa,Mheshimiwa

waziri ameamua kutoka na kwenda kujipumzisha sehemu tulivu.Mezani chupa kubwa ya mvinyo ilikuwa

imesimama .Dr maneno alikuwa amekaa peke yake akijaribu kuwazua hili na lile.hakutaka bughudha ya

aina yoyote ile.Wakati akiendelea kukata mvinyo taratibu simu yake inaita.Akaitoa mfukoni na

kuangalia.Alikuwa ni mheshimiwa Spika.
“Hallo mheshimiwa Spika”
“Mheshimiwa waziri uko wapi kwa sasa?
“Mimi niko sehemu Fulani napumzika.Kuna tatizo ganui mheshimiwa spika?
“Mheshimiwa waziri kuna tatizo kubwa linalomuhusu Mheshimiwa Roma.Hali yake bado si nzuri na

madktari wameshauri haraka sana apelekwe nje ya nchi.Kwa maana hiyo naomba ndani ya dakika kumi na

tano toka sasa tukutane hapo katika ofisi yangu ndogo.Fanya hima”
Kauli ile ya mheshimiwa Spika inamfanya mheshimiwa waziri wa afya nywele zimsisimke.
“Bastard!!!!!!!………..
“He’s still breathing….” Akanong’ona kwa ghadhabu Dr maneno.
“This cant be..” Akafoka tena kwa hasira.Akachukua simu yake na kupiga
“Halloo Mr Nkebo habari za saa hizi? Akasema Dr maneno huku amefura kwa hasira
“Habari nzuri Dr Maneno.Niko hapa na akina Faith,mheshimiwa Ngimarwa na wengine wote tunafurahia

ushindi wetu” Akasema Mr Nkebo huku akicheka kicheko cha chini chini.
“Mafurahia ushindi gani wakati mpaka sasa hivi Roma bado mzima? Bado anapumua na hivi saa Spika

kanipigia simu tuonane.Roma anatakiwa apelekwe nje ya nchi haraka iwezekanavyo.”
Kikapita kimya cha sekunde kadhaa halafu Mr Nkebo akasema kwa sauti kavu.
“Don’t let it happen.Roma must die tonight.Ukiacha Roma apelekwe nje ya nchi basi tumeumia.Kuna

mawili atapona na kuna hatari ikagundulika kuwa aliogea sabuni ya sumu.Uchunguzi ukifanyika

inaweza ikawa mbaya kwa upande wetu.Sasa fanya kila uwezalo,tumia madaraka yako yote kuhakikisha

kuwa Roma hapelekwi nje ya nchi.Ukifanikiwa kwa hilo basi Roma hafiki asubuhi.Ukiacha tu atolewe

nchini,tumekwisha.Do you understand that?
Dr maneno akapumua kwa nguvu kisha akajibu.
“I understand that.I wont let it happen……..”Akakata simu halafu kwa haraka akaelekea lilipo gari

lake akapanda na kuondioka kwa kasi.
Ili mchukua dakika kama kumi kuwasili katika ofisi ndogo ya spika.Usiku huu hakukuwa na

msongamanao mkubwa wa magari.Spika alikuwamo ofisini mwake akimsubiri.
“karibu sana mheshimiwa waziri.”
“Ahsante mheshimiwa Spika.Nimeitika mwito.Vipi hali ya bunge inaendeleaje? Akasema Dr maneno huku

akivuta kiti na kuketi
“Hali ya mbunge si nzuri na kila muda unavyozidi kwenda hali inazidi kuwa mbaya.Madaktari

wameshauri kuwa ili kuokoa maisha ya mheshimiwa roma inabidi haraka sana akimbizwe katika

hospitali kubwa nchini Israel.Suala la kumpeleka mgonjwa nje ya nchi lina taratibu zake za

kiserikali.Wewe ukiwa kama waziri wa afya una dhamana kubwa ya kuamua kuhusu wagonjwa wa kupelekwa

nje ya nchi.sasa nimekuita hapa ili tujadiliane kwa haraka nini cha kufanya ili mheshimiwa Roma

apelekwe nje ya nchi usiku huu.Kwa kuwa taratibu ni ndefu basi tunaweza andika kibali cha dharura

na usiku huu huu mbunge akapelekwa nje kwa matibabu halafu taratibu zingine zikafuatia wakati

tayari matibabu yanaendelea.”
Spika akamtazama Dr maneno aliyekuwa akisikiliza maelezo ya spika kwa makini .
“Mheshimiwa spika nafamu ni jinsi gani wote tulivyoguswa na tatizo hili la mheshimiwa

Roma.Ingekuwa ni kwa ridhaa yangu na yako hata sasa hivi mgonjwa angekuwa hewani akisafirishwa

lakini kuna taratibu za kiserikali ndizo hizo zinazoleta shida.Kusema ukweli kwa usiku huu mimi

siwezi andika kibali chochote labda hadi kesho ndipo ninaweza kuanza kulishughulikia suala

hili.Uliponipigia tu simu nimewasiliana na madkatari wa serikali ambao ni mabingwa wa moyo na

wamesema kuwa ugonjwa huo wa Mheshimiwa Roma unaweza kutibika humu humu nchini.Hakuina sababu ya

kumpeleke mgonjwa wa shinikizo la damu nje ya nchi wakati tunao wataalamu wetu wengi wa serikali

ambao ni mabingwa wa maradhi haya ya moyo.Hivi tunavyoongea maandalizi yanafanyika ili mheshimiwa

Roma ahamishiwe katika hospitali ya taifa ya muhimbili ambayo ina wataalamu wa hali ya juu

kabisa.”
Mheshimiwa waziri wa afya akasema kwa kujiamini.Spika akasimama na kumtazama Dr maneno kwa

hasira.hakutegemea katu kusikia jibu kama lile.
“waziri sijakuelewa vizuri,unasemaje?? Akauliza spika
“Nimesema hivi mimi kama waziri mwenye dhamana ya afya nimeagiza kuwa mheshimiwa mbunge ahamishiwe

katika hospitali ya taifa ya Muhimbili.Pale kuna wataalamu wa hali ya juu watakaoutibu ugonjwa

wake na tayari maandalizi yameanza kufanyika.Muda mfupi ujao nataka mheshimiwa mbunge ahamishwe

toka katika hospitali hiyo binafsi na kuhamishiwa katika hospitali ya serikali.Mbunge ni mtumishi

wa umma na hivyo atatibiwa katika taasisi za umma.Hospitali binafsi wao wanachofahamu ni pesa tu.”

Akasema Dr maneno kwa sauti iliyokuwa na aina Fulani ya ukali
Spika wa bunge akalengwa na machozi
“Siamini hayo unayoniambia Dr maneno.wewe unaelewa wazi kabisa uwezo mdogo wa hospitali zetu za

serikali na ndio maana wagonjwa wote wanapelekwa Tanzania heart hospital.sasa iweje leo uamuru

mheshimiwa mbunge ahamishwe toka katika hospitali ambayo inategemewa afrika mashariki na kati

umpeleke katika hospitali isiyo kuwa na uwezo wa juu katika tiba ya moyo?” Spika akauliza kwa

ukali
“Mheshimiwa Spika pale Muhimbili kuna kitengo cha moyo chenye mabingwa na hata wataalamu wa

kichina wako pale.Sioni tatizo lolote kwa mheshimiwa mbunge kutibiwa katika hospitali za

serikali.Mimi ndiye waziri wa afya na huo ndio uamuzi wangu.Nina imani pale atashughulikiwa na

madaktari wazalendo na atapona tu.”
“Ok nimekuelewa.we’re done in here.Unaweza kwenda.”
Waziri wa afya Dr maneno akatoka katika ofisi ya spika baada ya kuona tayari mheshimiwa spika

amekasirika.Spika wa bunge akafanya mawasiliano na mawaziri kadhaa lakini hakukuwa na hata mmoja

aliyeweza kumpa jibu lenye uhakika.Wote walisema wasubiri asubuhi ili waone ni jinsi gani ya

kulishughulikia suala hilo.Akatoka ofisini kwake na kumuamuru dereva wake kumpeleka hospitali

haraka iwezekanavyo.
Alipofika hospitali akafululiza kwa kasi hadi katika ofisi ya Dr Sandra.
“Dr mgonjwa anaendeleaje?”akauliza spika
“mgonjwa bado hali yake inazidi kuwa mbaya.Vipi umefikia wapi kuhusu suala lile?
“mambo magumu sana Dr.Nimetoka kuongea na waziri wa afya lakini tumshindwa kuelewana.Ameamuru Roma

ahamishiwe katika hospitali ya taifa ya muhimbili”
“Whaaaattttt!!!!????? …..akauliza Dr Sandra kwa mshangao.
“No its not true…These people are jocking” akalalama Dr Sandra
“Its not a joke Dr Sandra.Hivi tunavyoongea maandalizi yanafanyika na muda si mrefu mtatarifiwa

juu ya uhamisho huo”
Dr Sanra akamuangalia spika kwa macho makali.
“Mheshimiwa spika hivi mnajua mnachotaka kukifanya??
Spika hakujibu kitu.Dr Sandra akauliza tena.
“You are killing this young man…He’s going to die” machozi yakamlenga lenga
“Na wewe mheshimiwa spika umekubaliana na uamuzi huo?
“hapana sijakubaliana nao hata kidogo”
Dr Sandra akamtazama spika kwa makini sana halafu akasema.
“Mheshimwa Spika naomba unisikilize.Toka mheshimiwa Roma ameletwa hapa wewe ndiye kiongozi pekee

wa juu wa serikali uliyefika hapa na unayehangaika kuyapigania maisha ya mbunge huyu.Wewe ni

kiongozi jasiri.Ukiwa kama mzazi hutapenda kuona mbunge huyu kijana anafariki au kupata ulemavu wa

kudumu.Tukikubali hili litokee tutakuwa tumefanya kosa kubwa mno na pengo la kijana huyu

halitazibika kamwe.Kwa maana hiyo basi ninaomba kama kweli una nia ya dhati tushirikiane mimi na

wewe kuhakikisha kuwa hilo linalotaka kufanyika halifanyiki.Tuhakikishe mheshimiwa Roma ahamishiwi

Muhimbili na usiku huu huu anasafirishwa nje ya nchi.Are you ready for this?
Bila kusita spika wa bunge akajibu.
“Dr Sandra kwa kuyaokoa maisha ya kijana huyu niko tayari kwa lolote lile na hata kuhatarisha

maisha yangu,kazi yangu ilimradi Roma apone.”
“Good” Akasema Dr Sandra.Akamtazama tena spika halafu akasema
“Niliapa siku natawazwa kuwa daktari bingwa kuwa sintakubali hata siku moja kuona mgonjwa

akipoteza maisha kwa uzembe.Ndio maana ninapokuwa na mgonjwa huwa nafanya kila niwezalo

kuhakikisha namuhudumia hadi mwisho.Nimeumia sana moyoni kwa kitu anachotaka kukifanya waziri.Hii

inanipa picha ya wazi kuwa there is something going on here.”
“Kweli Dr Sandra haata mimi nimeanza kuhisi kitu kama hicho manake hii si kawaida.”
“Ok Usijali spika kwa vile umekubali kushirikiana na mimi basi napenda kukuhakikishia kuwa ndani

ya nusu saa ijayo tutamsafirisha mheshimwa mbunge.Litakalotokea litokee tu lakini bora tujaribu

kuliko kukaa na kusubiri kuhani msiba.Naomba sasa unisubiri hapo nje kama dakika tatu hivi”
Spika akatoka na kwenda kukaa katika masofa yaliyokuwa nje ya ofisi ya Dr Sandra.
Huku akipumua kwa nguvu Dr Sandra akachukua simu na kuzitafuta namba za baba yake Jeremy Mpama

raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.
“ Hallo Sandra how are you my love” Ilikuwa ni sauti nzito ya mheshimiwa Rais Jeremy Mpama.
“I’m ok dady how are you? Dr Sandra akauliza
“I’m ok.Mbona sauti yako inaonyesha kama una tatizo? Is there anything wrong my love” akauliza

mzee Jeremy
“Yes dady I have a problem.”
“My love,nimekwisha kwambia kuwa ,wakati niko hai duniani sintataka hata siku moja tabasamu

likauke usoni mwako.wewe ndiye binti wangu wa pekee na niko tayari kufanya lolote lile kwa ajili

yako”
Tabasamu likaanza kujengeka usoni mwa Dr Sandra baada ya kauli ile
“Niambie nini tatizo? Akauliza Rais
“Daddy tatizo ni kubwa lakini kwako wewe si kubwa na linahitaji kauli tu badala ya nguvu.” Dr

sandra akasema
“Mbona unashindwa kulisema tatizo gani linakusumbua my love.Sema tu mimi ndiye baba yako na

nitafanya kama unavyotaka.
“Daddy nafikiri una taarifa juu ya mbunge aliyepatwa na matatizo leo bungeni”
“Yes nimepewa taarifa zake.Nilizipata taarifa hizo nikiwa katika mkutano na mabalozi na hata hivi

ninavyoongea na wewe niko na mkutano na wakuu wa mikoa ya Mbeya ,Iringa na Rukwa.Nimekosa hata

muda wa kufuatilia anaendeleaje.Nilipewa taarifa kuwa ameletwa hapo hospitalini kwenu.”
“Yes daddy.Tumempokea mchana na tumekuwa tukiendelea kumuhudumia.Kusema ukweli daddy ugonjwa wake

ni mkubwa na anatakiwa haraka sana apelekwe nje ya nchi kwa uchunguzi zaidi.Mpaka sasa bado

hatujafanikiwa kulishusha shinikizo la damu Nimeongea na mheshimiwa spika nikamueleza naye

akaongea na waziri mwenye dhamana yaani waziri wa afya kuhusu kumpeleka nje mheshimiwa mbunge

lakini waziri wa afya amekataa katu katu na ameagiza mgonjwa ahamishiwe katika kitengo cha

magonjwa ya moyo cha hospitali ya Muhimbili.Daddy please understand me kama akihamishiwa kule he’s

going to die.I wont let him die just like that.I need to fight for him.Daddy naumia mno kuona

mgonjwa akiteseka hadi kufa kwa uzembe.Nimekwisha ongea na rafiki zangu wa hospitali ya Rambam

iliyoko Haifa Israel na wamekubali kumpokea mgonjwa.daddy I want to take him out of country in 30

minutes.”
“In 30 minutes?? Akauliza Rais
“Yes daddy and one more thing I need your plane” Dr Sandra akasema kwa sauti ambayo haikuwa na

masihara hata kidogo.
Kimya kikatanda.Mzee Jeremy alikuwa katika tafakari nzito.hakujua afanye nini.Ombi la mtoto wake

lilimstua mno.
“Daddy are you there? Dr Sandra akauliza baada ya kuona baba yake yuko kimya.
“I’m here love” Akajibu Raisa kwa upole
“natafakari uzito wa ombi lako.Kwa nini lakini us………………..”
Dr Sandra akakamkatisha baba yake aliyekuwa akitaka kuongea
“daddy No..this is not politics.This is life of someone.You promised to give me anything I

want.That’s what I want.I need your plane to take me to Israel in 30 minutes.Am I going to get it

or not? Kama haiwezekani niambie ili nijue nifanye kitu gani haraka.”
Dr Sandra akauliza kwa msisitizo
Mzee Jeremy alimpenda mno binti yake wa pekee na alikuwa tayari kufanya lolote lile kwa ajili

yake.Aliuona msisitizo aliouonyesha binti yake na akaona kuna kila ulazima wa kumsaidia.Hakupenda

kumuudhi binti yake.
“ Sandra my love ninaelewa ni kwa jinsi gani unavyoumia kuhusu suala hili.Japokuwa ni suala gumu

lakini ninakubali kubeba dhamana hii kwa ajili yako.Jiandae ndani ya muda huo unaoutaka utaondoka

na ndege yangu .Nitaongea na balozi wa Israel hapa nchini na kumweleza dharura hii iliyotokea,na

vile vile nitaongea na rais wa Israel na kumfahamisha juu ya suala hili ili usije ukapata usumbufu

wa aina yoyote ile.”
“Thank you so much daddy.You did great.Talk to you soon.I love you”
Dr Sandra hakutaka maongezi tena marefu na baba yake.Akatoka kwa kasi na kumkuta spika wa bunge

akimsubiri hapo nje ya ofisi yake.
“Mheshimiwa Spika.Kila kitu kiko shwari.Ndani ya muda mfupi ujao tutamsafirisha mgonjwa nje ya

nchi.”
“wow !! Dr Sandra “ Akasema Spika kwa furaha iliyochanganyika na mshangao.
Dakika kumi na tano tu zilitosha kabisa kumuandaa mgonjwa tayari kwa safari ya kuelekea nchini

Israel.Gari la wagonjwa lilikuwa tayari,mheshmiwa Roma akapakiwa na safari ya kuelekea uwanja wa

ndege ikaanza.
Uwanjani ndege ya Rais ilikwisha wekwa tayari kwa amri ya rais.Mgonjwa akaingizwa ndegeni tayari

kwa safari.Dr Sandra akamkumbatia spika kwa furaha.
“Nashukuru sana mheshimiwa Spika kwa kukubali kuwa upande wangu.Nakuahidi nitafanya kila niwezalo

kuhakikisha mheshimiwa mbunge anapona”
Wakaagana ,Dr Sandra akapanda ndegeni,milango ikafungwa na muda si mrefu ndege ikapaa
**********************************************************
Timu ya madaktari toka kitengo cha magonjwa ya moyo hospitali ya taifa ya Muhimbili kinawasili

katika hospitali ya magonjwa ya moyo ya Tanzania heart hospital ili kumuhamisha mheshimiwa mbunge

Roma kama walivyoamriwa na waziri wa afya.Taarifa waliyoipata toka kwa msemaji wa hospitali

zinawachanganya na kumlazimisha mkuu wa msafara ule ampigie simu waziri wa afya.
“Mheshimiwa waziri,kuna mambo yamejichanganya hapa.Taarifa tuliyoikuta hapa hospitali inasema

kuwa mgonjwa amesafirishwa nje ya nchi”
“Unasemaje??? Akahamaki mheshimiwa waziri
“taarifa toka kwa msemaji wa hospitali hii ni kwamba mgonjwa tuliyemfuata hapa Mheshimiwa Mbunge

Roma,amepelekwa nje ya nchi akiongozana na daktari mkuu wa hospitali hii Dr Sandra mpama na

muuguzi mmoja..”
“No….. haiwezekani…Nisubirini nakuja hapo sasa hivi”Akasema waziri
Jasho lilikuwa likimtoka.
“Lazima kuna kitu kimefanyika hapa.Watakuwa wamemficha mgonjwa .Si rahisi kumsafirisha mgonjwa nje

ya nchi bila mimi kujua.Mgonjwa ni laziam yuko humo humo hospitalini. Nitakwenda na kikosi cha

askari na kufanya upekuzi hospitali yote.Najua ni lazima atakuwa amefichwa katika moja ya vyumba

vya hospitali hiyo.”
Haraka haraka akapanda katika gari lake na kuodnoka kuelekea hospitalini ambako aliwakuta

madaktari toka hospitali ya muhimbili wakimsubiri.
Msemaji mkuu wa hospitali ile akamhakikishia kuwa mheshimiwa mbunge amesafirishwa nje ya

nchi.Bado hakuamini akaamua kumpigia simu mheshimiwa Spika.
“Mheshimiwa spika una taarifa zozote juu ya kusafirishwa kwa mbunge Roma nje ya nchi?”
“Ndiyo Dr Maneno.Nina taarifa hiyo na mimi mwenyewe nimewasindikiza na kuhakikisha ndege

imepaa.”
Sura ya mheshimiwa waziri ikazidi kujikunja kwa hasira
“Sikutegemea mheshimiwa spika kama na wewe unaweza ukashiriki katika uvunjifu huu wa sheria za

nchi.Unafahamu wazi kuwa zipo taratibu za kufuatwa lakini nyie kwa makusudi kabisa mmekiuka

mamlaka na kuchukua uamuzi wa kumtorosha mgonjwa kumpeleka nje ya nchi bila kibali cha

serikali.Hilo ni kosa mheshimiwa spika na utatakiwa kulijibu.”
“Mhshimiwa waziri nimefanya ninavyotakiwa kufanya.Hata watanzania wakisikia nilivyofanya

watanipongeza badala ya kunibeza.” Akasema spika kwa sauti ya kejeli
“Mheshimiwa spika umefanya kosa kubwa na itakubidi ulieleze bunge ni kwa nini umefanya kitu cha

namna hii.Kwa kuwa umeonyesha dharau kwangu mimi kama waziri mwenye dhamana ya afya naahidi kula

nawe sahani moja.Mheshimiwa utanisamehe kwa hili lakini ni lazima tupambane ili heshima iwepo.”

Akasema waziri kwa hasira
“Waziri usinitishe kabisa.Huna lolote la kunifanya.Nenda kanishtaki kokote unakoweza lakini uwe

tayari kueleza ukweli juu ya ajenda yako ya siri inayokulazimisha ufanye juu chini kuyahatarisha

maisha ya mheshimiwa mbunge.”
“Sema uatakavyo spika,lakini ni lazima nile na wewe sahani moja” Akasema waziri na kukata simu

kwa hasira.
“Damn you………………” Mheshimiwa waziri akapiga ukuta kwa hasira.akainama akatafakari halafu kwa

hasira akaelekea lilipo gari lake.Kabla hajalifikia gari lake simu yake inaita.Alikuwa ni kamanda

wa polisi dar es salaam.
“Mheshimiwa waziri nimekutumia vijana kumi na tayari wamekwisha fika hapohospitalini kama

ulivyoelekeza.”
“ahsante sana kamanda” waziri akajibu kwa mkato.Akageuka na kuangaa angaza getii ambaki aliliona

gari la askari likiwa limepaki.Akanyoosha mkono na kumuita kiongozi wa msafara ule.
“Kazi ya hapa imekwisha na hivi sasa tutaongozana kuelekea uwanja wa ndege” Akaamuru waziri.
Gari ya polisi ikiitangulia gari ya wairi zilikwenda kwa kasi ya ajabu kuelekea uwanja wa ndege

wa Julius Nyerere.Mheshimiwa waziri alikuwa amefura kwa hasira huku jasho likimtiririka.Alipofika

uwanjani alielezwa kuwa mheshimiwa Roma ni kweli amesafirishwa kwenda nje ya nchi kwa kutumia

ndege ya Rais kwa amri ya rais.
“This thing is more complicated than I thought” Akawaza mheshimiwa waziri wa afya huku

amejishika kiuno na jasho likimtiririka.Alikuwa akipumua kwa nguvu.Alihisi miguu inaihsha nguvu.

“wamefanikiwa kumsafirisha” Ilikuwa ni sauti y kiunyonge ya waziri wa afya akimfahamisha Mr Nkebo

katika simu.
“How could you let it happen Dr? Mr Nkebo akauliza kwa ukali
“Its complicated Mr Nkebo.It was an order from Mr President”
Mr Nkebo akapumua kwa nguvu.
“Unataka kuniambia rais ameshirikishwa katika hili?
“yah na ndiye aliyetoa ndege yake imsafirishe Roma.”Akasema waziri
Kimya kikapita halafu Nkebo akasema
“naona upepo umebadilika.Mchezo unaanza kuchezwa upya kabisa.hatuna jinsi safari hii ni lazima

tucheze na mheshimiwa rais”
“Mheshimiw Rais? Akauliza waziri
“yes Mheshimiwa rais” Akarudia tena Mr Nkebo.
“Nina imani kuwa huko aendako anaweza akapona.Atakapopona atakuja na nguvu mpya na mashambulio

makali japokuwa hatokuwa tena na ushahidi wa kutosha wa kutuhusisha sisi na benki ile.Lakini hilo

la kuharibu ushahidi bado halitoshi kutuhakikishia maisha ya utulivu,raha mstarehe.The guy is very

smart.Bado ataendelea kutufuata .kwa maana hiyo basi yatulazimu kujikinga mapema.Ni lazima

tumfanye mheshimiwa rais kuwa ngao yetu.Yeye ndiye mkuu wa nchi na akitukingia kifua basi hakuna

mwingine wa kutusumbua.”
“Mr Nkebo una mawazo mazuri sana,lakini bado sijakupata vizuri.How are we going to convince Mr

president to join us?” Akauliza waziri maneno
“ ahahahahaa its just simple Dr maneno.This is politics and you know what politics means.All

politicians are fighting for power so is Mr President”
“maneno yako yananipa matumaini makubwa Mr Nkebo.lakini bado nina wasi wasi kidogo na

kumshirikisha rais.”
“Dr Maneno usijali kabisa.Hilo ni jukumu langu na nitalifanikisha.Mimi ndiye nitakayekwenda

kuonana na rais.Kesho mheshimiwa rais anakuja Dodoma kwa vikao vya chama vitakavyoanza kesho

kutwa.Rais ananifahamu vizuri na akisikia niko Dodoma na ninahitaji kumuona basi atakubali haraka

sana.Sisi ndio wafadhili wa chama japokuwa hatutaki kujulikana moja kwa moja.Rais anatusikiliza

sisi.Nitaitumia fursa hiyo kutafuta kinga yake.”
“Nimekuelewa Mr Nkebo.Kama mtahitaji ushirikiano wowote toka kwangu msisite kunitarifu kwa

sababu sitegemei kuja Dododma hivi karibuni.mambo yaliyofanyika leo yamenitibua mno ,lakini

nimepata tumaini jipya kwa maneno uliyoniambia.”
“Usijali Dr maneno.Mimi ndiye Nkebo nisiyeshindwa na kitu chochote.See you then “
“good luck gentleman” akasema Dr maneno na kupumua kwa nguvu.tabasamu lenye Nuru likaanza

kujijenga tena usoni mwake.


“This is politics…………………..” Akanong’ona taratibu.




Wakati haya yote yakiendelea,katika ukumbi mdogo wa hoteli ya Dodoma palace hotel kikao kilikuwa

kikiendelea.Mbunge Damiani mwamba alikuwa ndiye mwenyekiti wa kikao hiki kilichowakutanisha baadhi

ya wabunge wa chama tawala na wenye nguvu bungeni na katika chama,pamoja na baadhi ya viongozi na

watendaji wa chama waliokuja mjini Dodoma kwa ajili ya vikao vya chama.
Damiani Mwamba alikuwa ni mmoja kati ya wabunge matajiri aliyewahi kushka nyadhifa mbali mbali

serikalini na katika chama.Amekuwa mbunge kwa miaka karibu ishrini sasa na bado wananchi wake

walikuwa wakimpenda na kumtaka aendeleee kuwasemea kama mbunge wao.Maendeleo aliyoyaleta jimboni

mwake yalikuwa ni ya kutiliwa mfano.Maji yalitiririka katika kila kijiji,bara bara zote zilikuwa

safi na zilizopitika kwa muda wa mwaka mzima bila matatizo,Zahanati zilijengwa katika kila

kata,umeme uliwaka katika kila kijiji .Alihmiza ujenzi wa viwanda vidogo vidogo vilivyoleta ajira

kwa mamia ya vijana,isitoshe aliwaleta wawekezaji wakubwa kuwekeza katika kilimo na uwekezaji

mkubwa.Haya ni baadhi tu ya mafaniko yaliyopatikana jimboni kwake na kumfanya awe ni mfano wa

kuigwa miongoni mwa wabunge.Ukaribu wake na Mheshimiwa Rais Jeremy mpama ulikuwa si wa kuulizwa

kwa sababu walisoma wote shule moja na huko ndiko walikoanzia shughuli za siasa.Kwa muda wa miaka

kumi na sita amekuwa waziri katika wizara mbali mbali hadi pale rais alipolivunja baraza lake la

mawaziri na yeye kuushangaza umma kutokurudi tena katika baraza la mawaziri.Hakuna ajuaye ni kwa

nini Mheshimiwa damian hakupewa uwaziri tena.Pamoja na kutopewa uwaziri katika serikali ,bado

mheshimiwa Damiana ameendelea kuwa na nguvu kubwa katika chama na bunge.Idadi kubwa ya viongozi wa

chama na serikali walikuwa upande wake.
“Ndugu wajumbe ,karibuni sana katika kikao hiki cha leo.Hiki ni moja tu ya vikao vyetu vya

kawaida ambavyo tutaendelea kukaa na kujadili mwenendo wa siasa hapa nchini.Kikao cha leo ni kwa

ajili ya kukumbushana baadhi ya mambo bila kusahau mkakatiwetu wa kuchukua urais katika uchaguzi

mkuu ujao ambao umekaribia sana.nawashukuru ndugu wajumbe kwa kazi kubwa na nzuri mliyoifanya na

mnayoendelea kuifanya kila siku.Nguvu yetu katika chama imeongezeka,idadi ya wajumbe wanaotuunga

mkono imeongezeka na hivyo kuzifanya mbio za kinyang’anyiro cha mgomea urais ndani ya chama kuwa

nyepesi sana kwa upande wetu.Nina imani tutashinda.Imani kwa wananchi na kwa wanachama imeongezea

na inaendelea kuongezeka licha ya kuwa kuna upinzani mkubwa kati yangu na rais.Vile vile kuna watu

ambao kidogo wanakuiwa ni tishio ingawa hawajaweka bayana dhamira zao za kugombea nafasi

hiyo.Mmoja waoni huyu kijana Roma.Kijana huyu ana nguvu sana katika jamii na hasa kwa vijana ambao

ndio wapiga kura wengi.Ikiwa ataweka nia ya kugombea kijana huyu ni tishio mno.Hatumuombei mabaya

lakini ikiwa kama atapona anaweza kuwa tishio kwetu.Lakini hawezi kutusumbua kwa sababu nguvu yake

katika chama bado ndogo.Kitu cha msingi kwa sasa ni kuanza kuchunguza wenzetu kambi ya rais

wanajiandaa vipi na nguvu yao ikoje.Mchakato huu ni lazima tuanze mapema sana.Sina wasi wasi na

utendaji wenu kwa sababu kazi yenu tayari inaonekana.Tunakotakiwa kuongeza nguvu kwa sasa ni kwa

wajumbe wa mikoani .Intakiwa tujiimarishe kule zaidi ii kusiwe na taizo la uungwaji mkono”
WHITE HOUSE ROMANCE SEHEMU YA SABA
ILIPOSHIA SEHEMU ILIYOPITA
Dr Sandra akahisi kijasho kikimtoka baada ya taarifa ile ya Dr Jacob.Akakohoa kidogo kutafuta

sauti halafu kasema
“Dr Jacob nashukuru kwa kazi kubwa mliyoifanya na ugunduzi mliogundua.Kwa ufupi tu ni kwamaba

huyu mgonjwa ni mwanasiasa.Ni mbunge ambaye anapendwa na watu wengi .Kupendwa huko kumemfanaya awe

na maadui wengi vile vile.Nina imani hata sumu hiyo iliwekwa makusudi na maadui zake kisiasa.Dr

Jacob naomba mfanye kila linalowezekana ili mgonjwa huyu apone kwa sababu ni tumaini la

wengi.Naomba vile vile asiruhusiwe mtu yeyote kuja kumuona mgonjwa zaidi yangu mimi au

nitakayemruhusu kwa sababu watu hawa waliofanya hivi hawatasita kumfuata Roma hadi huku .”
“Usihofu kitu Dr Sandra.Hopitali yetu ina usalama mkubwa na hakuna mtu yeyote anayeweza kuja

kufanya kitendo chochote kibaya hapa.hata hivyo tutafanya kama ulivyoomba na hatutamruhusu mtu

yeyote kwenda kuonana na mgonjwa.Kwa sasa operesheni inaandaliwa na baada ya masaa mawili tutakuwa

tumeanza na tutakutaarifu kila kitu kitakavyokuwa kikiendelea.Naahidi kumshughulikia mgonjwa huyu

kwa kila namna tunayoweza ili apone kwa heshima yako.Hospitali yako na yetu zimekuwa marafiki kwa

muda mrefu sasa,kwa hiyo naomba uwe na amani ya moyo”
Dr Sandra akatabasamu ,akaagana na Dr Jacob akatoka kuelekea madukani kwa ajili ya kujinunulia

vitu vichache vya kutumia kwa muda atakaokuwa hapo Haifa


ENDELEA...........................................................................................

.


Ni saa mbili za usiku katika ikulu ndogo mjini Dodoma rais wa Tanzania Mzee Jeremy Mpama akiwa na

rafiki yake mkubwa ,mfanya biashara maarufu na kada wa chama Mr Nkebo, katika bustani ya ikulu

ndogo .Walikuwa wakipata chakula cha usiku huku wakibadilishana mawili matatu.Ni mr Nkebo ndiye

aliyeomba kuonana na Mzee Mpama kwa usiku huu .Jeremy Mpama hakuweza kukataa ombi la Mr Nkebo kwa

kuwa ni mmoja kati ya watu muhimu na anaowaheshimu sana.Ni kwa sababu ya kutambua umuhimu wake

ndio maana usiku huu rais alivunja ratiba zake ili kupata wasaa wa kuonana na kada huyu wa chama
“Mr President tumepotezana sana siku za karibuni” Akasema Mr Nkebo huku ajimimnia mvinyo katika

glasi yake
“Ndiyo Mr Nkebo kwa miezi kama mitatu mine iliyopita imekuwa ni kipindi cha kazi nyingi

kwangu.Nimekuwa na ziara nyingi za kimataifa na ndio maana nimekuwa sipatikani mara kwa mara.Leo

uliponipigia simu kuwa uko Dodoma na ukaomba kama nina nafasi tuonane nilifurahi sana kwa kuwa ni

muda hatujaonana.Vipi biashara zinaendaje?
“Mr President biashara zinakwenda vizuri licha ya kushuka kwa thamani ya shilingi na kuongezeka

kwa bei ya mafuta katika soko la dunia bado tunafanya biashara nzuri” Akasema Mr Nkebo
“Hilo la kushuka kwa thamani ya shilingi yetu linatuumiza vichwa mimi na viongozi wenzangu

serikalini.Nina imani tutafanikiwa kuifanya shilingi yetu iwe na thamani tena”
“ndiyo Mr Pesident nakuamini utafanikiwa katika hilo.Naamini kwa watu uliowapa dhamana ya

kulishghulikia suala hiloni wachapa kazi hodari .”
Mzee Jeremy akacheka kidogo akainua glasi yake ya mvinyo nakupiga funda dogo.
“Mr President vipi upepo wa kisiasa unakwendaje ?manake naona vuguvugu la urais limeanza kupamba

moto”
“Yah! Mr Nkebo upepo wa kisiasa si mbaya japokuwa kuna changamoto nyingi na vikwazo vingi

lakini sina wasi wasi na kuteuliwa tena na chama changu kugombea urais kwa awamu ya pili”
“Hata mimi Mr president sina wasi wasi na hilo lakini kwa hali tuliyopanza kuiona kwa sasa

inaonekana hamasa ya kuwania uteuzi hii imeongezeka sana ndani ya chama.Japo hatujui bado nani na

nani wana nia ya kuwania uteuzi huo lakini tayari dalili zimekwisha anza kujionyesha na ni dhahiri

unaweza ukakumbana na upinzani mkali sana.”
“Nakubaliana na wewe Mr Nkebo upinzani utakuwepo.Lakini hebu nipe picha halisi ya upepo

unavyouona Mr Nkebo kwa sababu wewe ni mshauri wangu mzuri sana katika mambo kama haya”
Sura ya Mr Nkebo ikapambwa na tabasamu pana.Akainua glasi yake akapiga funda kubwa halafu

akasema.
“Mr President tayari ndani ya chama kuna watu wamekwisha anza kutengeneza makundi ya kuhakikisha

kuwa wanashinda katika uteuzi huo.” Kauli ile inamfanya Mzee Jeremy kujiweka sawa na kumsikiliza

Mr Nkebo kwa makini.
“jana usiku nilipata taarifa toka katika moja ya vyombo vyangu vya taarifa kilichokuwapo katika

kikao kimoja cha siri kilichoendeshwa katika hoteli ya Dodoma palace .Mr Damian Mwamba tayari

amekwisha anza mbio za kuwania uteuzi huo.Na kwa taarifa zenye uhakika tayari amekuwa na uungwaji

mkono wa kuridhisha toka kwa wajumbe.Timu aliyoiteua ifanye kazi hii inafanya kazi yake kwa

umakini na usiri mkubwa na kusema ukweli hawalali.Wanafanaya kazi usiku na mchana.Mr Damian

hajaanza mbio hizi jana wala juzi.Ameanza kitambo sana.Wakati akitafuta uungwaji mkono katika

miongoni mwa wajumbe wa chama ,amekuwa pia akijijengea jina katika jamii.Kwa hivi sasa jina la Mr

Damiani linatajwa sana katika orodha ya watu weye sifa na uwezo wa kuiongoza nchi hii.Amekuwa

akitoa misaada mbali mbali katioka mashule,kwa wanafunzi,vikundi vya akina mama na vijana,amejenga

mashule na kila linapotokea suala lolote la ktaifa amekuwa mstari wa mbele sana.Si kwamba

namuhofia Mr Damiani lakini kwa kasi anayokwenda nayo ndiyo iliyonisukuma kutaka kuonana na we ili

tujadili kwa kina kuhusu suala hili.”
Mheshimiwa Rais akapumua kwa nguvu na kumuangalia Mr Nkebo usoni.Alionyesha uoga wa dhairi kwa

maneno yale aliyoambiwa. Nkebo akanywa tena funda lingine la mvinyo halafu akaichukua chupa na

kumimina tena mvinyo katika glasi yake.Mzee Jeremy alikuwa kimya kabisa.
“Mr president,wewe ni rafiki yangu,umeshanisaidia katika mambo mengi sana kwa hiyo kunapokuwa na

suala lolote lile ambalo ninajua si zuri kwa upande wako ni lazima nikwambie.Kuna kitu umekifanya

jana ambacho kwa kweli lilikuwa kosa ingawa hukulifahamu.Ni kuhusu yule mbunge Roma.nadhani

utakuwa umepata wasaa wa kutazama televisheni kuanzia jana na kuona ni jinsi gani suala la ugonjwa

wake limeviteka vichwa vya watu.Mr President yule kijana ni tishio kubwa kwa sasa.Ugonjwa wake huu

wa ghafla umenistua mno baada ya kuona ni jinsi gani anavyopendwa na watu.Sikufichi mheshimiwa

rais yule kijana ana nguvu kubwa katika jamii.Nchi yote ilizizima baada ya taarifa kusambaa kuwa

amefariki dunia.Kasi anayokuja nayo inaleta wasi wasi mwingi.Kijana huyu atakuwa na hatari kubwa

iwapo atataka agombee urais.Kwa mujibu wa marekebisho ya katiba yaliyofanywa,tayari Roma

anaruhusiwa kikatiba kugombea urais.Na nina imani kuwa hiyo ndiyo nia yake kwa sababu huko mitaani

anadiriki kuitwa rais wa wanyonge.Naelewa nguvu yake katika chama si kubwa lakini anaweza

kushawishiwa kujiunga na chama pinzani ili agombee urais na kama akifanyua hivyo mheshimiwa rais

basi shughuli itakuwa ngumu.Kuna uwezekano mkubwa kijana yule akatwaa nchi.Mheshimiwa rais kosa

ulilolifanya ni kutoa ndege yako kumsafirisha Roma na kuyaokoa maisha yake.Ilitakiwa kijana yule

afariki dunia jana.kama angeondoka usoni pa dunia jana ile basi uwanja wa mapambano ya uras

ungetuhakikishia ushindi upande wetu.”
Mheshimiwa Rais akatoa kitamba ana kujiuta jasho lililoanza kumtoka.akatwaa glasi yake akapiga

funda kubwa na kumgeukia Mr Nkebo.
“Kweli leo nimeamini Mr Nkebo wewe n rafiki yangu wa kweli.Hakuna katika watu wangu wa karibu

aliyekuja na kunieleza mambo uliyonieleza leo.hakuna hata mmoja aliyeweza kugundua hatari iliyoko

mbele yetu.Nashangaa hata hawa washauri wangu wa mambo ya siasa ni kwa nini wamekaa kimya wakati

kumbe kuna hatari kubwa inatukabili.Nadhani hata hawa washauri wangu watakuwa tayari

wamesharubuniwa na ndio maana wamekaa kimya na kusubiri kuanguka kwangu.Kuhusu yule kijana Roma

mimi sikuwa nimejua kama ni kijana hatari.Iwapo ningejua kama ana nguvu ndani ya jamii basi

nisingekubali kutoa ndege yangu impeleke huko Israel akatibiwe.Vile vile lilikuwa ni ombi maalum

la Binti yangu.Unajua Mr Nkebo mimi nina mtoto mmoja tu na mara nyingi huwa sipendi kumuona akiwa

na huzuni moyoni.Yeye ndiye furaha yangu .kwa maana hiyo nilimuahidi kumpa chochote atakachohitaji

ili kumrudishia furaha yake.Alichokiomba ilikuwa ni ndege yangu na sikuweza kumkatalia kwa sababu

nilikwisha muahidi.Kutokana na majukumu mengi yanayonikabili nashindwa kupata muda hata wa

kufuatilia mambo ya siasa yanavyokwenda nchini .mambo yote yanayohusu mwendendo mzima wa siasa

nimeyakabidhi kwa washauri wangu wa mambo ya siasa.Wameniudhi mno.Haiwezekani wakashindwa kuwa na

taarifa kama hizi wakati kila kitu wanacho.Nimewapa nguvu na kuwawezesha kwa kila kitu ili

kuhakikisha kuwa bado ninaendelea kuwa na nguvu na hatimaye kupata ridhaaya kuongoza tena kipindi

kijacho.Ahsante sana Mr Nkebo kwa taarifa yako.Hapa nilipo nahisi kuchanganyikiwa sijui hata

nifanye kitu gani” Akasema Mzee Jeremy.Huku akitabasamu Mr Nkebo akasema
“Mr President usipate shida yoyote mimi nipo nitakuelekeza nini cha kufanya kama utakuwa tayari

kufuata ushauri wangu”
“Kwa nini inifuate ushauri wako Mr Nkebo wakati wewe ndiye uliyekuja kunifumbua macho? Nielekeze

nifanye nini.Tena kuanzia sasa ningeomba uwe ndiye mshauri wangu wa siri wa mambo haya ya siasa.”
“kama nilivyokwisha kueleza Mr President mimi nipo hapa na niko tayari kukushauri na hatimaye

kuhakikisha kuwa unashinda katika awamu ijayo .Lakini kazi hii siwezi kuifanya mimi peke yangu

.Kitu cha kwanza tunachotakiwa kukifanya ni kuunda timu ndogo ya watu ambayo itafanya kazi ya

kuchunguza mwenendo wa siasa na kuangalia nini tufanye ili tuweze kupata ushindi ambayo itakubidi

mheshimiwa rais uiwezeshe ili iweze kufanya kazi zake kikamilifu bila kugundulika.Timu hii itakuwa

ya watu sita ambao nitakupa majina yao.Ni watu ambao inakupasa uwaamini kwa sababu ni wataalamu

katika michezo hii ya kisiasa.Kitu cha pili ambacho tutakifanya baada ya kuunda timu hii ni

kuwanyamazisha wale wote wanaoonekana kuwa na nguvu kisiasa na kuhatarisha urais wako kwa kipindi

kingine.”
Mzee Jeremy akamtazama Mr Nkebo halafu akauliza.
“Kuwanyamazisha kivipi?
“Mr resident politics is a dirty game and to win this game you need to play dirty too” Akasema Mr

Nkebo.
“Bado sijakuelewa Nkebo hebu nifafanulie vizuri”
“Mheshimiwa rais ninaposema kumnyamazisha mtu yeyote mwenye kuwa na nguvu kisiasa nina maana ya

kumpunguzia nguvu yake aliyonayo na wakati mwingine ikibidi hata kumuondoa katika uso wa dunia hii

iwapo kutakuwa na ulazima wa kufanya hivyo.Kazi hii si kazi rahisi ,inahitaji umakini na wataalamu

wa hali ya juu mno ndiyo maana nikasema inabidi tuwezeshwe ili kufanikisha shughuli kama hizi.Kwa

kuanzia ,tutaanza na wale ambao tayari wamekwisha onyesha wazi dhamira zao za kuwania urais kama

Mr Damian na huyu kijana Roma.Sisi tutawashughulikia bila hata ya mtu yeyote kuhisi kuwa unahusika

kwa namna yoyote na wao.Ninakuhakikishia Mheshimiwa rais kuwa hakuna mtu atakayejua nini

tunakifanya “
Sura ya mheshimiwa rais ikajenga tabasamu pana baada ya uchambuzi wa kina wa jinsi mambo

yatakavyoendeshwa ili kuwamaliza wabaya wake kisiasa.Mpaka wanamaliza maongezi Mzee Jeremy

akamkabidhi rasmi Mr Nkebo jukumu zima la kuhakisha kuwa wale wote wanasiasa wanaoonekana kuwa na

nguvu ndani na nje ya chama na ambao wanaonyesha dhamira ya wazi ya kugombea urais wanamalizwa

kimya kimya.Rais alimuahidi Nkebo kumuwezesha yeye na kamati yake kwa kila kitu

watakachohitaji,kama vile ulinzi na fedha.Saa saba za usiku Mheshimiwa Nkebo akatoka maeneo ya

ikulu ndogo akisindikizwa na walinzi maalum kuelekea katika hoteli aliyopanga.
Siku ya tano toka mheshimiwa Roma ameletwa katika hosopitali hii ya Rambam medical center mjini

Haifa Isarel.Operesheni aliyofanyiwa ili kuondoa sehemu za mwili wake zilizokuwa zimeharibiwa na

sumu ,ilifanikiwa .Madaktari walifanikiwa kuyaokoa maisha ya mbunge Roma.Dr Sandra Mpama hakuweza

kuizuia furaha aliyonayo baada ya kufanikiwa kupambana na kuokoa maisha ya mgonjwa.Kwake huo

ulikuwa ni ushindi mkubwa.Siku zote amekuwa ni mtu wa kuyapigania maisha ya wagonjwa wanaopelekwa

katika hospitali yake hadi mwisho.Moyoni alijipongeza kwa ujasiri aliokuwa nao wa kuweza

kumsafirisha Roma nje ya nchi japo kuwa alikumbana na vikwazo vingi.
Hali ya Roma ilikuwa ikiendelea vizuri siku hadi siku.Licha ya hali yake kuonyesha maendeleo

mazuri ,bado alikuwa katika uangalizi maalum wa kidaktari na kwa muda huo wote hakuna

aliyeruhusiwa kuonana naye.Dr Sandra alikuwa akipewa taarifa mara kwa mara juu ya maendeleo ya

mgonjwa wake.Siku hii Roma aliamka vizuri mchangamfu na anayeweza kuongea vizuri.Madaktari

wakampima na kuona kuwa tayari hakukuwa na hatari yoyote inayomkabili,Dr Sandra akapewa taarifa

kuwa sasa anaweza kuoanana na mgonjwa na bila kuchelewa akaenda hospitalini hapo.Alimkuta Roma

ameaala kitandani
Daktari aliyekuwa akimuhudumia Roma akamtambulisha Dr Sanndra.
“Roma huyu ni Dr Sandra Mpama toka katika hospitali ya moyo ya Tanzania heart hospital.Ni yeye

ndiye aliyekuleata hapa siku ile ukiwa hujitambui.Kwa kiasi kikubwa yeye ndiye shujaa

aliyefanikiwa kuyaokoka maisha yako kwa sababu baada ya kuona kuwa ugonjwa wako ulikuwa mgumu

kutibika katika hospitali yao ikabdii fanye uamuzi wa haraka haraka wa kukuleta huku .Tunamshukuru

mno dokta huyu kwa ujasiri wake.”
Roma alikuwa akitabasamu asiyaamini macho yake.Alikuwa akifahamu kwa kifupi kuwa ugonjw

auliokuwa ukimsumbua ni shinikizo la damu lakini Hakuwa ameambiwa ni jinsi gani alivyofika pale

katika hospitali ile na ni nani aliyempeleka.Alitamani ainuke na kwenda kumkumbatia Dr Sandra

mwokozi wake lakini hakuwa bado na nguvu za kuweza kufanya hivyo.
Dr Sandra aliiona furaha aliyokuwa nayo Roma na kwa kuwa hakuwa na nguvu za kuinuna akamfuata

pale kitandani ,akamkumbatia huku naye machozi yakimtoka akiwa haamini kama ni kweli kijana yule

kipenzi cha wengi alikuwa amepona.
“Thank you God” Akamshukuru Mungu.
“Dr Sandra sijui nikushukuruje kwa namna ulivyoyaokoa msiaha yangu.Wewe ni daktari wa kweli” Roma

alisema huku naye machozi yakimlenga lenga.
“Usijali Roma haya yote ni maongozi ya Mungu.yeye ndiye anayepanga kila kitu kiwe.Sifa zote na

utukufu tumrudishie yeye”
Dr Sandra akaenda kukaa katika kiti kilichokuwa pembeni ya kitanda.Kwa sasa walikuwa wawili tu

chumbani.Dr Sandra yeye alikuwa akiipitia ripoti ya madaktari kuhusu maendeleo ya mgonjwa lakini

Roma bado aliendelea kumtaama Dr Sandra kwa makini.
“Dr Sandra nafurahi mno kukuona .Nilipopata fahamu na kugundua kuwa siko nyumbani nilijiona

mkiwa sana.Sikujua kama ulikuwa uko hapa na mimi.Kwa sasa unakaa wapi? Roma akauliza
“Kwa sasa ninakaa Leonardo hotel” Dr Sandra akajibu.
“Nani anakulipia gharama za hoteli na kila kitu? Roma akauliza tena
“Gharama zote ninalipa mwenyewe? Sandra akajibu huku akitabasamu .Roma akamwangalia kwa mshangao.
“Unalipa mwenyewe? Akauliza.
“Ndiyo mheshimiwa ninalipa mwenyewe.Kwani kuna ubaya wowote?
“hakuna ubaya Dr Sandra ,ila kwa kawaida gharama hizi hulipwa na serikali .”
Dr Sandra akacheka kidogo halafu akasema
“Usijali mheshimiwa Roma.Mimi nitalipa tu si gharama kubwa za kunishinda.”
“Ina maana serikali hawajui kama nimefuatana na wewe huku? Roma akauliza
“Mheshimiwa Roma kuna mambo mengi ya kuongea lakini kwa sasa naomba ujitahidi kwanza upone ,upate

nguvu za kutosha halafu tutakaa na kuongea.
Huku akitabasamu Roma akasema
“Dr Sandra huku tuko ugenini hivyo naomba mambo ya uheshimiwa tuyaweke pembeni.Niite Roma

inatosha.”
Dr Sandra akatabamu na kumuendea Roma pale kitandani.
“Dr Sandra ulisema unaitwa Sandra Mpama?
“Ndiyo. Sandra Mpama? Akajibu Sandra huku akitabasamu
“Are you related in anyway with Mr Jeremy Mpama ?
Kicheko kidogo cha chini chini kikamtoka Dr Sandra
“He’s my father”Akajibu kwa ufupi
“Your father??? Roma akauliza kwa mshangao
“yes.He’s my father.”
Roma akakaa kimya kidogo.
Kumbe ni mtoto wa Rais.Sura yake si ngeni machoni mwangu.Ni kama nimeshwahi kumuona

sehemu.Nadhani tumeshakutana mara kadhaa katika dhifa za kitaifa ikulu.Sasa nimeshapata picha kuna

kipindi niliwahi kusikia kuwa kuna hospitali kubwa na nzuri ya maradhi ya moyo imefunguliwa

inaongozwa na mtoto wa rais.baadhi ya watu walikuwa wakihoji alikoweza kupata fedha za kujenga

hospitali hiyo kubwa na ya kisasa.Hospitali hii ndiyo iliyoniokoa.Daktari wake ndiye aliyeyaokoa

maisha yangu..Lakini kuna kitu bado kinanisumbua akiliyangu.Iweje niletwe huku Israel kwa

shinikizo la damu,ugionjwa ambao hospitali zetu nyumbani zina uwezo wa kuutibu? Japokuwa

ninaendelea vizuri lakini nahisi ni kama upotevu wa fedha za serikali.Au kuna ugonjwa mwingine

mkubwa na wanashindwa kuniambia? Yawezekana kuna kitu wananificha.Haiwezekani nipoteze mamilioni

ya fedha kwa ajili ya kutibiwa shinikizo la damu nje ya nchi.lakini kama ni ugonjwa mwingine

visitors comments